Header Ads Widget

BARAZA LA UMOJA WA AFRIKA LAOMBA SUDAN IONDOLEWE VIKWAZO

 


Baraza la Amani na Usalama la Jumuiya ya Afrika limetaka Baraza la Usalama la UN mnamo tarehe 15 Agosti, kuanza taratibu

kuondoa marufuku ya silaha kwa Sudan Kusini ili kusaidia nchi hiyo kushughulikia changamoto zake za usalama, kituo cha Eye Radio kimesema.

Baraza hilo lilisema hatua hiyo itawezesha Sudan Kusini "kudumisha umoja na nguvukazi muhimu", kituo hicho kiliripoti.

"Pia lilitoa wito kwa washirika wa kimataifa kuondoa vikwazo vilivyowekwa dhidi ya nchi ili kuwezesha utekelezaji wa haraka wa makubaliano ya msingi ya [amani ya 2018]", Redio hiyo ilisema.

Baraza hilo pia lilielezea wasiwasi juu ya kuzorota kwa hali ya kibinadamu nchini humo, vurugu kati ya jamii, ukosefu mkubwa wa usalama wa chakula, uhamishaji wa ndani na ufikiaji mdogo wa misaada ya kibinadamu katika maeneo yaliyoathirika na vita.

Lilitaka mashirika ya misaada na Sudan Kusini kushughulikia maswala hayo.

Pia lilionyesha wasiwasi juu ya "kuwekwa kizuizini kwa makamu wa rais wa kwanza Riek Machar na mvutano wa kisiasa uliopo", Eye Radio iliripoti.

Baraza hilo lilitoa wito Machar kuachiliwa huru mara moja na bila masharti, pamoja na kutatuliwa kwa mgogoro wa kisiasa nchini.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI