Header Ads Widget

JINSI TRUMP ANAVYOTAKA MAREKANI KUNUFAIKA KUTOKANA NA MKATABA WA AMANI WA CONGO


Utawala wa Trump unaongoza mpango kabambe, lakini wenye utata, wa amani unaolenga kumaliza mzozo wa muda mrefu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ambao pia unajumuisha nchi jirani ya Rwanda.

Juhudi zake za upatanishi hazishangazi, kwani DR Congo - taifa lililo katikati mwa Afrika - limejaliwa kuwa na utajiri wa madini ambao Marekani inahitaji kuendesha Teknlojia ya mawasilaino (IT), na sasa Akili Mnemba (AI),ambayo kwa kiwango kikubwa kwa sasa yanakwenda China.

Rais wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kuwa mwenyeji wa viongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda - Félix Tshisekedi na Paul Kagame - katika wiki zijazo ili kutia saini makubaliano ya amani ambayo ameyataja kama "ushindi mtukufu", akitumai kuunga mkono na mikataba ambayo itaongeza uwekezaji wa Marekani katika eneo hilo.

Mkurugenzi mtendaji wa wakfu wa World Peace yenye makao yake nchini Marekani Prof Alex de Waal aliiambia BBC kwamba utawala wa Trump unakuza "mtindo mpya wa kuleta amani, unachanganya utendaji na makubaliano ya kibiashara".

"Trump amefanya hivyo nchini Ukraine pia. Anataka kutumia mpango huo kukuza hadhi yake ya kisiasa, na kupata madini kwa maslahi ya Marekani," Prof De Waal alisema.

 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI