Header Ads Widget

WAZIRI MKUU KUFUNGA MAONYESHO YA MADINI KESHO MKOANI LINDI

  

NA HADIJA OMARY 

LINDI..

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa anatarajiwa kufunga maonyesho ya Madini awamu ya pili katika mkoa wa Lindi wilaya ya Ruangwa.

Akizungumza na waandishi wa habari,mkuu wa wilaya ya Kilwa Mohamed Nyundo alisema kuwa waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa ambaye ni mbunge wa jimbo la Ruangwa mkoani Lindi atafunga maonyesho madini ambayo yameonyesha fursa mbalimbali.

Nyundo alisema kuwa mkoa wa Lindi umebarikiwa kuwa na ardhi yenye madini mbalimbali tofauti na mikoa mingine hapa Tanzania.


Alisema kuwa anawakaribisha wadau mbalimbali wa madini kwenda kuwekeza katika sekta ya madini mkoani Lindi kwa kuwa ni mkoa wenye usalama wa kutosha.


Nyundo alisema kuwa kutokana na maonyesho ya Madini yametoa fursa mbalimbali na kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo kuwa wakubwa na kukuza uchumi wa wananchi wa mkoa wa Lindi na Tanzania.








Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI