Header Ads Widget

RONALDO KUCHEZA BRAZIL? APOKEA NONO

 

Mshambuliji wa Al-Nassr Cristiano Ronaldo, 40, amepokea ofa kutoka kwa klabu ya Brazil ambayo haijafichuliwa, ambayo ingemruhusu nyota huyo wa Ureno kucheza Kombe la Dunia la Klabu ya Fifa litakaloanza Juni. (Marca - kwa Kihispania)

Aston Villa inavutiwa na mshambuliaji wa Barcelona Ferran Torres, 25, na ipo tayari kutoa takriban euro milioni 50 (£42m) kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania. (Mundo Deportivo)

Manchester United imewasilisha ofa ya euro milioni 65 kumsajili mshambuliaji wa Brentford na Cameroon Bryan Mbeumo, 25, ambaye amesalia na mwaka mmoja kwenye mkataba wake wa sasa. (Fichajes)

Winga wa Lyon mwenye umri wa miaka 21 Mfaransa Rayan Cherki, anayewaniwa na Manchester United na Liverpool, amethibitisha kuwa ataondoka katika klabu hiyo ya Ufaransa msimu huu wa kiangazi. (Goal)

Manchester United pia inataka kumsajili kiungo wa Sporting na Ureno Pedro Goncalves, 26, msimu huu wa kiangazi. (Team talk)

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI