Header Ads Widget

RIGATHI GACHAGUA: 'KAMA NIMEFANYA UHALIFU WAJE NYUMBANI KWANGU KUNIKAMATA'

Rigathi Gachagua

Aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua nchini Kenya ameithubutu serikali kumkamata ikiwa ametenda uhalifu wowote.

Akihutubia wanahabari Jumatatu mjini Karen, Nairobi, Gachagua alionekana kujibu kauli tofauti za Naibu Rais Kithure Kindiki na Waziri wa Mambo ya Ndani Kipchumba Murkomen kwamba hawezi kuguswa na atakamatwa kwa madai ya matamshi yake ya uchochezi.

Alisema yeye wala wafuasi wake hawataogopa au kutishwa na matumizi ya mfumo wa haki ya jinai.

"Kama serikali inajua kwamba nimefanya uhalifu unaojulikana chini ya sheria za Kenya na kutambuliwa ndani ya kanuni ya adhabu, wanajua nyumba yangu ilipo ... na, niko hapa, wanajua nyumbani kwangu wamunyoro," alisema.

"Mchezo wa kutafutana barabarani unapaswa kukoma."

Alisema maafisa wa usalama badala yake wanapaswa kumfuata nyumbani na kuchukua hatua inayofaa.

Gachagua alikwepa maafisa wa polisi huko Muranga na kuelekea nyumbani kwake Wamunyoro huko Nyeri huku polisi wakimfuatilia.

Maafisa wanaofahamu operesheni hizo walisema hawakumpata usiku

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI