Makamu wa Rais wa Marekani J.D. Vance amesema mazungumzo ya kumaliza vita nchini Ukraine yamefikia "mkwamo mdogo" na maafisa wa Marekani wanafahamu hilo, Reuters inaripoti.
"Putin haonekani kujua jinsi ya kutoka kwenye vita hivi," Vance aliongeza.
Makamu huyo wa rais alikariri kuwa ikiwa Urusi haiko tayari kushiriki mazungumzo, Marekani itajiondoa kwenye mchakato huo, kwa kuwa hivi sio vita vyake.
Vance alitoa kauli hizi chini ya saa moja kabla ya simu iliyopangwa kati ya Donald Trump na Vladimir Putin.
0 Comments