Header Ads Widget

NCHI ZA NORDIC NA SUA KUIMARISHA USHIRIKIANO.

 

 Na Lilian Kasenene,Morogoro

Chuo  Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo SUA kimeendelea kuimarisha ushirikiano na nchi za Nordic kwenye nyannja mbalimbali ikiwemo ya kubadilisha Walimu na wanafunzi.

Makamu mkuu wa Chuo hicho Cha SUA Prof.Raphael Chibunda alieleza hayo mara baada ya mabalozi wa nchi za Sweden, Norway, Denmark, na Finland kutembelea chuoni hapo na kufanya majadiliano juu ya ushirikiano walionao wa muda mrefu.


Prof. Chibunda alisema serikali na wananchi wa nchi hizo wamekuwa na ushirikiano wa muda mrefu ambapo alitolea mfano wa nchi ya Norway ambayo ilikuwa ya kwanza kuhamasisha taaluma ya degree ya misitu na imeendeleza kusaidia katika mambo mengine mbalimbali na nchi ya Denmark ilikuwabya kwanza katika kusaidia ujenzi wa jengo la ndaki ya tiba ya wanyama   katika Chuo hicho.

"Tumewashukuru na Sasa tumeendelea kusimama kwa nguvu zetu wenyewe na Walimu wetu wenyewe na kumeweza kukipanua chuo kwa sababu ukiangalia wakati wanasaidia kilikuwa na idadi ndogo ya wanafunzi wasiozidi 2,000  ukilinganisha na Sasa ambapo wapo wanafunzi zaidi ya 18,000,"alisema.

Alisema ujio wa nchi hizo walikuja kuona wanaendelezaje na na kwamba utaendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano zaidi pamoja na kubadilishana wanafunzi na Walimu wabobezi,wandamizi ili wanafunzi waweze kupata uzoefu zaidi.

Aidha makamu mkuu huyo alieleza kuwa nchi ya Norway kupitia Shirika lake la Maendeleo la NORAD Wana mpango wa kutangaza nafasi na kuweka fedha za utafiti hivyo kama Chuo kupitia watafiti wake watahakikisha wanawahamasisha kuchangamkia fursa hiyo na kuwaandaa na ni imani yake kuwa kwa weledi na uzoefu walionao wanaweza kupata baadhi ya miradi.


Balozi wa Denmark nchini Tanzania Jesper Kammersgaard alisema amefurahishwa kutembelea SUA pamoja na mabalozi wenzake, vyuo vya nchi hizo wataendeleza mashirikiano zaidi.

"Mashirikiano haya kwa nchi hizi za Nordic na nchi ya Tanzania ni wa zaidi ya miaka na miaka tumefurahi sana Sisi kama mabalozi,"alisema balozi huyo.

Katika hatua nyingine balozi huyo wa Denmark Jesper, akizungumza kwa niaba ya mabalozi wenzake wakiwa katika Ushirika wa Wahitimu wa Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo SUA-(Sokoine University Graduate Entrepreneurs Cooperative (SUGECO), alipongeza Tanzania kutokana na matokeo chanya waliyobaini kwenye sekta ya Mifugo,kuwajengea Uwezi vijana kujiajiri.

Alisema pamoja na eneo la misitu waliahidi ushirikiano zaidi ambao utaelekea kwenye maeneo ya nidhati jadidifu,tafiti,Kilimo na Maendeleo ya jamii.

Mkurugenzi wa SUGECO Revocatus Kimario alisema kazi wanazofanya kwa ushirikiano na nchi za Denmark,Norway, Sweden na Finland ni kuona mikakati wanazofanya na moja wapo ni kuwapeleka vijana kwenye nchi husika ambapo mpaka sasa vijana 850 kwa miaka miwili wamepelekwa, 2023-vijana 535 walipelekwa na wanaendelea kupelekwa.

Pia alisema kwa sasa wako kwenye mikakati wa kuanzisha kituo Cha umahili Cha uzalishaji wa mbegu za nguruwe kwa Morogoro kwa kushirikiana na kampuni za Denmark.

Ziara hiyo ya mabalozi mkoani Morogoro wametembelea pia kituo Cha kuzalisha mbegu za miti kilichopo chini ya Wakala wa Misitu Tanzania(TFS) ambapo walishiriki upandaji miti.



MWISHO 

SIMULIZI CHINI⬇️⬇️⬇️⬇️


Apata kazi ya mshahara mnono huku akiacha pombe baada ya miaka 10 

Kijana mmoja aitwaye Musa alianza kunywa pombe mapema mwaka 2014 akiwa katika shule ya upili, hii ni kutokana na shinikizo la rika lake, hivyo akajikuta kila wikiendi anakunywa pombe kwa siri katika baa za mtaani kwao. 

Baada ya miaka nane pombe ikawa imekolea kwenye damu yake, kichwa chake na moyo wake, huku mkewe Salome akizoea kula Sukumawiki wiki nzima maana mumewe fedha zote anazimalizia kwenye pombe. 

Mtoto wake mwenye umri wa miaka mitano bado hajaanza shuleni kwa sababu ya kukosa fedha, mkewe anachoweza kufanya ni kununua chakula cha mtoto pekee ila suala la shule hawezi kumudu gharama zake. 

Kusema kweli maisha ya Musa yamekumbwa na urahibu wa pombe, unajua urahibu ni aina ya utumwa, unajikuta unatoa ahadi kwamba utaacha lakini baada ya muda unajikuta tena katika ulevi huo. 

Ndivyo yalivyo maisha ya Musa yeye si mteja tena katika Baa ya Hashtag huko Rombo, yeye ni mbia, mtu mashuhuri na mteja mwaminifu wa Baa hiyo kwa miaka mingi. 

Hata hivyo, ilikuwa mshtuko mkubwa kote Rombo wakati Musa alipata kazi yenye malipo mazuri, huku akiachana kabisa na pombe ambayo imeharibu maisha yake kwa miaka mingi. Lakini ilikuwaje akapata ushindi huo?. 

Musa alikutana na mwanafunzi mwenzake wa zamani ambaye naye kama yeye alikuwa amekunywa pombe bila kukoma tangu mwaka 2018 ila aliacha kutokana na matibabu bora ya mitishamba kutoka kwa Kiwanga Doctors. 

Basi alimpa Musa mawasiliano ya Kiwanga Doctors na maelekezo ya muhimu, alifka kwa wataalamu hao na mara moja walishughulikia tatizo lake. 

Ndani ya mwezi mmoja tu, Musa alisema siku za giza katika maisha yake zimekwisha. Mkewe alisherehekea hatua hiyo kubwa kama vile ameshinda bahati nasibu ya mamilioni ya fedha. 

"Mimi na pombe tumeachana rasmi na sitaki kurudi nyuma, ninataka kuijenga familia yangu, wameteseka vya kutosha. Asante sana kwa Kiwanga Doctors kwa kunisaidia kushinda ulevi na kuniwezesha kupata kazi nzuri," alisema Musa. 

Vilevile Kiwanga Doctors wana uzoefu wa miongo kadhaa ya kutibu kwa kutumia dawa kali za mitishamba kuponya magonjwa kama shinikizo la damu, kisukari, vidonda vya tumbo, kisonono, kaswende, TB, miguu kuvimba au kuwaka moto n.k. 


Hushughulikia matatizo ya jumla kuanzia kushinda kesi za mahakama, kushinda bahati nasibu, ulinzi wa familia na mali na hutabiri kwa usahihi nyota.
Ni watu wengi hadi sasa wamepata mafanikio, uponyaji na furaha kupitia huduma za Kiwanga Doctors ambao unaweza kuwasiliana na kwa namba  +255 763 926 750  au tembelea tovuti yao, maelezo zaidi kuhusu huduma zao ambazo zimewasaidia wengi. 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI