Header Ads Widget

MAREKANI YAZITAKA INDIA NA PAKISTAN KUPUNGUZA HALI YA WASIWASI BAADA YA MAUAJI YA KASHMIR

 
Marekani imezitaka India na Pakistan kufanya kazi pamoja ili "kupunguza hali ya wasiwasi" baada ya shambulio baya la wanamgambo katika eneo la Kashmir linalotawaliwa na India wiki iliyopita kuwaua raia 26.

Waziri wa mambo ya nje Marco Rubio alifanya mazungumzo tofauti na waziri wa mambo ya nje wa India na waziri mkuu wa Pakistan siku ya Jumatano na kuwataka "kudumisha amani na usalama katika Asia Kusini".

India inaishutumu Pakistan kwa kuunga mkono wanamgambo baada ya shambulio la Aprili 22 kwenye eneo la karibu na mji wa mapumziko wa Pahalgam.

Islamabad inakanusha madai hayo. Siku ya Jumatano India pia ilitangaza kufungwa kwa anga yake kwa ndege zote za Pakistani, katika msururu wa hatua za piga nikupige zilizochukuliwa na pande zote mbili.

"Wahusika, waungaji mkono na wapangaji" wa shambulio la Pahalgam "lazima wafikishwe mbele ya sheria", Waziri wa Mambo ya Nje wa India S Jaishankar aliandika kwenye X baada ya kuzungumza na mwenzake wa Marekani kwa njia ya simu, huku Rubio akielezea masikitiko yake na kuthibitisha uungaji mkono wa Washington katika mapambano ya India dhidi ya ugaidi.

Wakati huohuo, mwanadiplomasia mkuu wa Marekani alieleza haja ya "kulaani shambulio la kigaidi" katika mazungumzo yake na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif. Aliitaka Islamabad kushirikiana "katika kuchunguza shambulio hili". Wakati wa mawasiliano hayo ya simu, Sharif alikataa "majaribio ya Wahindi kuhusisha Pakistan na tukio hilo", taarifa iliyotolewa na ofisi yake ilisomeka.

Waziri Mkuu wa Pakistani pia aliitaka Marekani "kuishinikiza India kufuta matamshi hayo na kuchukua hatua kwa uwajibikaji".

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI