Header Ads Widget

WATU WANNE WAUAWA, 43 WATEKWA KASKAZINI MAGHARIBI MWA NIGERIA

 


Polisi katika Jimbo la Katsina kaskazini magharibi mwa Nigeria, wamesema watu 43 wametekwa nyara katika kijiji kimoja, huku wengine wanne wakiuawa katika shambulio baya.

Inakuja chini ya wiki moja baada ya Jenerali wa Jeshi la Nigeria kuachiliwa baada kuzuiliwa karibu miezi miwili na watekaji nyara.

Katsina, jimbo analotoka Rais wa zamani wa Nigeria Muhammadu Buhari, limeshuhudia mashambulizi ya mara kwa mara ya majambazi na watekaji nyara ambayo yamegharimu maisha ya watu wengi.

Katika shambulio hilo la Jumapili usiku, wakaazi walisema kuwa watu wanaoshukiwa kuwa majambazi waliokuwa wakiendesha pikipiki waliwavamia wakaazi wakiwapiga risasi kabla ya kuwateka nyara waathiriwa.

Baadhi ya wanakijiji walipigwa risasi na kusababisha vifo vya watu wanne huku wengine wengi wakijeruhiwa.

Polisi wanasema msako unaendelea ili kuwaokoa waathiriwa na kuwakamata wahusika.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI