Header Ads Widget

WATAALAMU WA KIMTANDAO WAKUTANA ARUSHA,WAJADILI NAMNA YA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZA KIMTANDAO.



Na Pamela Mollel,Arusha 

Wataalamu wanaohusika katika  usalama wa  mitandao kutoka Tanzania na nje ya Nchi wamekutana katika  jukwaa la nne la  pamoja la kujadiliana namna ambavyo mifumo itakuwa mathubuti katika kukabiliana na changamoto za kimtandao Duniani 

Akizungumza katika jukwaa la nne,Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama Tanzania Dkt Nkundwe Mwasaga anasema kuwa  wamekuwa wakikutana na wataalamu  wa mitandao kutoka Tanzania na Nje ya nchi ili waweze kujadiliana na kuweka maazimio ya kuboresha  usalama  wa mitandao .


Ameongeza kuwa kila ifikapo Aprili ya kila mwaka wamekuwa wakikutana na wataalamu wa mitandao ili kuweza kubadilishana utaalam pamoja na kupeana mrejesho wa mambo mbalimbali 

"Eneo la usalama wa mitandao ni eneo ambalo linabadilika kila wakati hivyo ni muhimu kuwa na mifumo mathubuti"Ameongeza Dkt.Mwasaga


Kwa upande wake Afisa Usalama mtandao kutoka Benki ya CRDB,Robert Karamagi anasema kuwepo kwa makongamano kama hayo itasaidia Tanzania kuwa makini na wale wadukuzi wa mitandao

"Kwa namna ambavyo teknolojia ya mitandao inakuwa kwa kasi kubwa inahitajika elimu kwa jamii kujua namna ya kukabiliana na tishio lolote la kimtandao 

Naye mtaalamu wa usalama mtandao na uchunguzi wa makosa mtandaoni Yusuph Kileo akiwasilisha mada ya uhalifu wa mitandaoni anasema kuwa  jukwaa hilo ni muhimu kwani linajadili changamoto  za kimitandao na kuzitafutia uvumbuzi.


Anaongeza kuwa tafiti zinaonyesha kuwa uhalifu mitandaoni unagharimu Dunia Dola Trilioni 10.5 kila mwaka hali ambayo inaogopesha

"Taasisi nyingi zinakumbana na changamoto za kimtandao ikiwemo kuibiwa taarifaa au fedha"Anasema Kileo 

Mtaalamu wa mifumo ya Tehama kutoka IPP media Eng.Moses Fumbuka anasema kuwa  kazi nyingi zinafanyika kupitia mifumo kwa asilimia 90

"Kwa hali ilivyo sasa huwezi kufanya chochote hivyo ni muhimu kuelewa mifumo inavyofanya kazi lakini hasa usalama wa mifumo "Anasema Eng.Fumbuka

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI