Header Ads Widget

VIFAA VYA UPELELEZI VYA URUSI, VYATISHIA USALAMA WA UINGEREZA - TIMES

 


Vyanzo vitatu katika Wizara ya Ulinzi ya Uingereza vililiambia jarida Sunday Times kwamba kabla ya uvamizi kamili wa Ukraine, kulikuwa na habari za kuaminika kwamba maboti ya kifahari yanayomilikiwa na mabilionea wa Urusi oligarchs yanaweza kuwa yalitumika katika upelelezi chini ya maji kote nchini Uingereza.

Baadhi ya vyombo hivi vina madimbwi ya maji ambayo yanaweza kutumika kwa siri kuweka na kupata vifaa vya upelelezi na kupiga mbizi kwenye kina kirefu cha bahari.

Kulingana na gazeti hilo mlipuko wa Nord Stream umeonyesha kuathirika kwa mfumo wa usambazaji wa nishati ya Uingereza: nchi hiyo inapokea karibu theluthi moja ya umeme wake kutoka kwa mitambo ya upepo ya pwani kupitia nyaya za chini ya maji.

Mabomba ya mafuta na gesi, ambayo yanaweza kuzimwa kwa malipo ya chini ya maji, yanaweza pia kuwa hatarini.

Nyaya za mtandao, ambazo maeneo yao yanajulikana, pia zipo hatarini.

Hatahivyo, vyanzo vya Jeshi la Wanamaji vinasema kampuni za kibinafsi zinazotunza nyaya hizi zimeweka hifadhi kubwa ya nyaya hizo hali ya kwamba mfumo umejengwa kwa ustahimilivu wa kutosha kuhakikisha kuwa unajinasua kwa haraka kutoka kwa shambulio.

Lakini kinachosumbua zaidi jeshi ni uwezo wa Urusi wa kuchora ramani, kushambulia au kuharibu nyaya za kijeshi.

Jeshi la Wanamaji la Uingereza sasa linapendekeza mpango mpya kwa jina "Atlantic Bastion" ili kuunda magari ya angani, ardhini na chini ya maji pamoja na sensa ili kulinda maji ya Uingereza na eneo lote la Atlantiki ya Kaskazini.

Vilevile, baadhi ya maafisa wa jeshi la wanamaji wanaamini Uingereza inahitaji kupiga hatua zaidi na kurejesha uwezo wake wa kutega mabomu ya ardhini, jambo ambalo haijafanya tangu kumalizika kwa vita baridi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI