Header Ads Widget

SENSA ZA UPELELEZI ZA NYAMBIZI YA NYUKLIA ZAPATIKANA KATIKA PWANI YA UINGEREZA

 


Sensa zilizofichwa zimegunduliwa katika maji ya Uingereza, ambapo jeshi linashuku ziliwekwa na idara ya ujasusi ya Urusi kuzichunguza nyambizi za nyuklia za Uingereza zilizobeba silaha za nyuklia.

Sensa hizo zilizogunduliwa na jeshi la Uingereza zilionekana kuwa tishio kwa usalama wa taifa

Waandishi wa habari wa taarifa hiyo pia walipata fursa ya kuingia katika meli inayofanya upepelezi baharini ya Royal Navy kwa jina Proteus, ambayo inafanya kazi katika maji ya Uingereza.

Hii ni mara ya kwanza kwa raia kuruhusiwa kuingia kwenye meli hiyo ya siri, ambayo ilizinduliwa 2023, iliongeza taarifa hiyo.

Kama gazeti hilo linavyosema, Urusi ndiyo nchi pekee yenye kundi la nyambizi maalumu kwa ajili ya vita vya baharini na ujasusi.

Kulingana na taarifa hiyo, baadhi ya uwezo wa nyambizi hizo unavuka uwezo wa Uingereza na washirika wake wa NATO.

Takriban nyaya 11 za intaneti zimeharibiwa katika Bahari ya Baltic katika kipindi cha miezi 15 iliyopita, zingine zikiangusha nanga na kupelekea baadhi ya watu kuzishuku meli za Urusi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI