Rais wa Marekani Donald Trump amepuuzilia mbali madai kwamba usitishaji wa utekelezaji wa ushuru mpya ulilenga kuzinusuru baadhi ya nchi.
Akiandika kwenye mtandao wa kijamii Trump alisema: "Hakukuwa na ubaguzi wa ushuru uliotangazwa Ijumaa."
Rais alisisitiza kuwa bidhaa za kielektroniki kutoka Uchina bado zilikuwa chini ya ushuru wa 20% unaohusiana na dawa ya fentanyl - lakini sasa walikuwa kwenye "kikapu tofauti cha ushuru".
Kwa muda mrefu Marekani imekuwa ikishutumu mashirika ya Kichina kwa kusambaza kwa makusudi vikundi vilivyohusika katika uundaji wa opioid ya syntetisk ambayo ilizua shida ya dawa nchini.
Trump alisema kuwa uchunguzi ujao kuhusu ushuru na usalama wa taifa utaangalia bidhaa za elektroniki kama vile semiconductors na "msururu mzima wa usambazaji wa vifaa vya elektroniki".
Alirejelea nia yake ya kurudisha viwanda Marekani, akiandika "Kilichofichuliwa ni kwamba tunahitaji kutengeneza bidhaa nchini Marekani".
Trump alisema hii ni ili kuepuka "kudhibitiwa" na nchi, ikiwa ni pamoja na China ambayo alielezea kama "taifa la kibiashara lenye uadui"
0 Comments