Header Ads Widget

KENYA: WANAWAKE 129 WALIUAWA KATI YA JANUARI NA MACHI MWAKA HUU

 


Kati ya mwezi Januari na Machi 2025, Kenya ilikumbwa na janga kubwa la mauaji ya wanawake, ambapo jumla ya wanawake 129 waliripotiwa kuuawa.

Mnamo Januari, wanawake 43 waliuawa, wakifuatiwa na 42 mnamo Februari, na 44 mnamo Machi.

Maeneo ya Bonde la Ufa, Mashariki, na Magharibi yaliandikisha idadi ya juu zaidi ya vifo hivyo.

Takwimu zinaonyesha kuwa wanaume walihusika na asilimia 85 ya mauaji haya, huku wanawake wakihusishwa na asilimia 10.

Katika visa vingi, wahalifu walikuwa watu waliowafahamu waathiriwa, na nusu ya mauaji haya yalihusiana na migogoro ya kifamilia.

Kwa mwaka wa 2024 pekee, jumla ya visa 579 za mauaji ya wanawake ziliripotiwa.

Taarifa hizi ni kwa mujibu wa Huduma ya Kitaifa ya Polisi pamoja na Kituo cha Kitaifa cha Utafiti wa Uhalifu.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI