Header Ads Widget

RC KIHONGOSI AWAPONGEZA TANROADS, TARURA ASISITIZA THAMANI YA MIRADI IONEKANE.

MKUU wa Mkoa wa Simiyu Kenani Kihongosi (aliyesimama) akiongoza kikao cha Barabara kilichofanyika ukumbi wa Bariadi Conference.


Na Costantine Mathias, Bariadi,


MKUU wa Mkoa wa Simiyu Kenan Kihongosi leo 04 Machi, 2025 ameongoza kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Simiyu katika ukumbi wa mikutano wa Bariadi.


Akizungumza wakati wa kufunga kikao hicho, Kihongosi amewapongeza Wakala wa Barababara Nchini TANROADS  pamoja na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini TARURA kwa kazi nzuri wanayofanya ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Amewasisitiza Wakala wa Barabara Nchini TANROADS pamoja na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini TARURA, kuhakikisha wanalipa madeni ya wakandarasi  wanaotekeleza miradi ya barabara ili kuharakisha ukamilikaji wa miradi   kwa wakati.


Aidha amewataka kuhakikisha kuwa miradi inayotekelezwa Mkoani Simiyu inalingana na thamani ya Fedha.


Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoani Simiyu hufanyika  mara mbili kwa  Mwaka kutathmini utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Barabara.


Mwisho.






Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI