Header Ads Widget

HATIMAYE NDOTO YA GRACE MAYEMBA YA KUJENGA SHULE YA SEKONDARI, CHUO NA HOTELI YAANZA KUTIMIA


Na Matukio Daima Media,Njombe

Grace Mayemba, Ambaye Kwa Sasa Anafanya Kazi Ya Kufundisha Lugha Ya Kingereza huko Nchini Taiwani Amefanikiwa Kufikia Malengo Yake Ya Muda Mrefu Ya Kusaidia Watoto Wa Kitanzania Wanoishi Kwenye Mazingira Magumu Yanayowakwamisha Kupata Elimu Na Maarifa Katika Vijiji Mbalimbali Hapa Nchini. 


Grace Anasema Wazo La Kujenga Shule Na Chuo cha Ufundi Hapa Nchini Lilitokana Na Changamoto Alizozibaini Kuwepo Kwenye Jamii Tangu Alipoanza Masomo Yake Ya Shule Ya Msingi Katika Kijiji Cha Mkongotema Wilayani Madaba Mkoani Ruvuma Mwaka1988 [Kwa Sasa Magingo Baada Ya Kijiji Mama Kugawanywa]Na Kisha Kujiunga Na Sekondari Ya Ya Wilima Ambako alihitimu Kidato Cha Nne Mwaka 1998 Na Baadae Akajiunga na Shule ya Sekondari Ya Kulipia Ya Mpechi Kwa Masomo Ya Kitato Cha Tano Na Sita Mkoani Njombe mwaka 1999- 2000 Ambako Hakufanikiwa Kuhitimu Kutokana Na Kukosa Ada Na Michango Mingine

 


Kutokana Na Ugumu Wa Maisha Kusoma Kwa Kumtegemea Mama Yake Pekee Kwa Kuuza Pombe Ya Kienyeji Aina ya Ulanzi Grace Alienda Kuishi Kwa ndugu Yake Jijini Dar es salamu Ambapo Badae 

Akajiunga Chuo na Cha Ualimu Vikindu Mkuranga Mkoani Pwani Na Kisha Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania Tawi la Kinondoni Biafra Ambako Alisoma Huku Akifanya Kazi Ya Ualimu Wa Shule za Msingi za serikali. 

 

Anasema Kwa Sehemu Kubwa Amejisomesha Yeye Mwenyewe Kwa Kufanya Shughuli na kujituma Kwa Kufanya Kazi Mbalimbali za kujiingizia kipato tangu akiwa Shule Ya Msingi Mpaka Chuo Kikuu Huku Akiwa amebeba Ndoto Kubwa Ya kujikwamua kimaisha yeye na Jamii Ya Watanzania wenye hali kama yake.

 

‘’Nilisoma Kwa Shida Sana Baba Yangu Alifariki Nikiwa Darasa La Tano Shule Ya Msingi Akiwa Ametuacha Watoto Saba Pamoja Na Mama Nilipojiunga Shule Sekondari Wilima Kidato Cha Kwanza Hali IlikuaNgumu Sana Ikanilazimu Kufanya Vibarua Vya Hapa Na Pale Ili Kupata Ada Na Mahitaji Mengine’’Alisimulia Grace Mayemba.

 


Garace akifanya kibarua cha kusomba tofali huko kijiji cha mkongotema Baadae Grace Alijiunga Na Masomo Ya Masters Nchini Taiwani katika chuo kikuu cha National Tsing Hua 

Akisomea Lugha[ Masters of Linguistics ] Ambako Alihitimu mwaka 2023, pia alifanyia utafiti ya masomo yake kwenye lugha ya a Kibena yenye mada ya ‘Tense Aspect and Modality in the Bena Language’. Na Kisha Kupata Kazi ya kufundisha katika Moja Ya Shule Za Kiingereza za mfumo wa kimarekani Huko 

Taiwani.

 


Picha Ni Grace Mayemba akiwa na furaha Baada Ya Kuhitimu Masomo Ya Shahada Ya Uzamiri [Masters] Hukonchini Taiwan aliyoisotea kwa miaka 


Katika Ndoto Yake Grace Anasema Aliweka nadhiri Kuwa aKifanikiwa Kwenye Maisha Yake Atahakikisha 

Anajenga Shule Ambayo Itasaidia Mtoto Wa Kitanzania Kupata Elimu Katika Mazingira Rafiki Na Kwa Gharama Nafuu Ndoto Ambayo Imeanza Kutimia Ambapo Kwa Sasa Ameungana Na Rafiki Zake kutoka Taiwani akiweno Winnie , Professor Perng, na Wataiwani Wengine Kujenga Shule Ya Msingi ya Mchepuo Wa Kiingereza Na Chuo Cha Ufundi Stadi pamoja na hoteli Katika Kijiji Cha Magingo Wilayani Madaba Mkoani Ruvuma . 


Shule Hiyo Pia Itasaidia Kupunguza Idadi Kubwa Ya Wanafunzi Katika Shule Za Msingi Za Serikali Huku Chuo Kikitarajiwa Kupunguza Idadi Ya Vijana Wasio Na Ajira Baada Ya Kupata Ujuzi Wa Fani Mbalimbali Hususani wale ambao hawata Weza Kuendelea Na Masomo Ya Juu. Chuo Kitatoa Mafunzo Ya Hoteli , Kompyuta, Utalii, Umeme, Ufundi Bomba, ushonaji, Uandishi wa Habari, Ualimu wa chekechea na Kutakua na Kozi Nyingine Zinazoweza Kuwapa Ujuzi Watanzania Kuweza Kuajiriwa Na Kujiajiri kutokana na uhitaji. 



Kwa Kuanza Grace Na Rafiki zake Wameanzisha Mradi Wa Kufanikisha Ndoto Hiyo Kubwa Unaoitwa Alpha Tanzania Little dreamers’ big futures, Ambapo Katika Mradi Huo Kuna Wadau Mbalimbali WanaoJitolea Kufanikisha Ujenzi Wa Shule Hiyo Na Chuo cha ufundi Katika Kijiji Cha Magingo Wilayani Madaba Mkoani Ruvuma Hapo February 28 Mwaka 2025 Wadau Kutoka Nchini Taiwani Na Tanzania Kutoka Mikoa Mbalimbali Wamefanya Kikao Cha Kwanza Kwa Njia Ya Mtandao Kujadili Mambo Kadhaa Mhimu Ikiwemo Historia Ya Wazo La Kujenga Shule [Ndoto Ya Grace] Kueleza Mradi Mzima Ulipo Fikia, Na Kuwasilisha Wazo La Kujitolea kwa wadau hao Kikao Ambacho Kilikua Na Washiriki Nane ambao kwa pamoja walionyesha nia ya kuhakikisha ndoto hiyo kubwa ya muda mrefu inafanikiwa kwa ukaubwa wake kama kama yalivyo matamanio ya dada grace na rafiki zake. 


Alpha Tanzania Kama Mradi Kwa Sasa Utakuwa Na Safu Ya Wafanyakazi Wa Kujitolea Na Viongozi Kutoka Nchi Hizo Mbili Ambapo Grace Jenipher Mayemba Anakuwa Ni Mkurugenzi mkuu Wa Mradi Kutoka Tanzania, Winnie  Mkurugenzi Wa Mradi Kwa Nchi ya Taiwan, Ben Lin Mkuu wa Idara ya Fedha Na Elimu, Kelly Mkuu wa Idara ya Tehama Na Angle kwok mkuu wa Idara ya ubunifu na Matangazo upande wa Taiwani. Mpaka Sasa Mradi Wa Alpha Tanzania Umefikia Hatua Nzuri Ambapo Umesha Pata Eneo La Kujenga Shule Ya Msingi Ya Mchepuo Wa Kingereza Kijiji Cha Magingo eneo la kihoho Na Chuo Cha Ufundi eneo la ukubwa wa ekari kumi. Mradi Umepata ufadhili kutoka kwa Mr .Chen (陳炘陽 ) wa Kufikisha Umeme Na Maji Kutoka Kijijini Mpaka Eneo La Ujenzi [Sight] Na Kujenga Msingi Wa Madarasa Sita Ya Shule Ya Msingi.

 

‘’Tulipo Fika Kijiji Pale Magingo Mimi Na Rafiki Zangu Kelly Na Winnie Tuliwaeleza Lengo La Kujenga Shule Na Tukapewa Eneo La Kujenga Shule La Ukubwa Ekari 10 Ambalo Tulilitembelea Na Kuona Linafaa Kujenga Shule Ya Msingi Chuo Na Hoteli’’Grace

 


Kwa Mujibu Wa Grace Mayemba Jitihada Za Kufanikisha Ndoto Na Kupata Fedha Zinaendelea Kupitia Wadau Kutoka Nchini Tanzania Na Taiwani Ambapo Anasema Anatamani Ndoto 

Hii Itimie Mpaka Ifikapo Mwaka 2030 Kwa Kujenga Shule Ya Msingi Mchepuo Wa Kiingereza ,Chuo Cha Ufundi Stadi Na Hoteli Katika Eneo Alilopewa Bure Na Serikali Ya Kijiji Cha Magingo Huko Mkoani Ruvuma Nchini Tanzania Mradi Ambao Unakadiriwa Kugharimu Zaidi Ya Shilingi Bilion Mbili Za Kitanzania.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI