Header Ads Widget

DKT. MWINYI KUFUNGUA TAMASHA LA UWEKEZAJI MICHEWENI PEMBA


RAIS wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi anatarajia kufungua Tamasha  la Tatu la Uwekezaji Zanzibar linalorajia kufanyika  Mei 07 na 08 mwaka huu  Micheweni  Pemba.

Tamasha hilo litahusisha Wawekezaji wa Ndani na Nje ya Nchi, Viongozi wa Wafanyabiashara, Taasisi za Umma na Binafsi.

Akitoa taarifa kwa Waandishi wa Habari Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi, Uchumi na Uwekezaji Shariff Ali Sharif amesema kuwa, Tamasha hilo ni kichocheo cha mabadiliko  ya kiuchumi na kuweka Pemba kuwa kituo cha Uwekezaji wa Kimataifa.

Amesema lengo kuu la Tamasha hilo ni kuitangaza Pemba kuwa kisiwa cha kuvutia Uwekezaji katika madhari ya uchumi wa Zanzibar.


Amefahamisha kuwa kwa sasa Pemba ina fursa kubwa ya Uwekezaji hivyo Serikali imejidhatiti kuhakikisha wanaweka mazingira bora na kuwavutia Wawekezaji kuwekeza  kisiwani Pemba na kufungua fursa nyingi za ajira kwa vijana.

"Tamasha hili linaashiria mwanzo wa enzi mpya ya upanuzi wa kiuchumi na kuonesha fursa kubwa za zilizopo kisiwani Pemba katika Sekta mbalimbali na kuchangia ongezeko  la ajira na kuboresha maisha ya waakazi wake," ameeleza.

"Katika Tamasha hili kutakuwa na jukwaa litakalo weka mkakati wa wa kupata fursa za ushirikiano wa moja kwa moja kati ya Wawekezaji, Viongozi wa Biashara na taasisi za Serikali na Binafsi," amefafanua

Aidha ameeleza kuwa, Kutakuwa na Mjadala ambao utaangazia mifumo ya Sera na mikakati inayolenga kuboresha urahisi wa kufanyabiashara Zanzibar  pamoja na kukuza maendeleo jumuishi.

Amefafanua kuwa, Serikali ya Mapinduzi  ya Zanzibar  inaendelea kuweka mazingira  mazuri ya biashara yanayoyanufaisha Wawekezaji  na Wananchi kwa Ujumla.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI