Header Ads Widget

ASKOFU DR KIPANGULA AKEMEA VIJANA KUENDESHA MAISHA KWA KUBETI NA LBL

 

Na Leonard Johnson ,Matukio Daima Media Iringa 

ASKOFU wa kanisa la kiinjili la  kilutheli Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mufindi Dkt.Antony kipangula Amewataka vijana kuacha kutegemea kutafuta pesa kupitia mitandao ya simu kama Kubeti  na LBL  badala yake wajikite   kufanya kazi ambazo zinaweza kuwaingizia  kipato halali.

Kuwa Kasi ya Vijana na baadhi ya watanzania kushinda kwenye mitandao kutafuta pesa ni kubwa Kuliko Ile ya kufanya kazi za uzalishaji mali kama Kilimo na nyingine .

Askofu Dkt Kipangula alisema ni vema mitandaoni kuingia baada ya kutoka Shamba kulima na isiwe kazi ya kuingiza kipato .


Askofu Dkt Kipangula alisema hayo Jana wakati wa Ibada ya uzinduzi wa Jimbo la  Nyanyembe   wilaya ya Mufindi  Mufindi  Mkoani Iringa na kumuingiza kazini mkuu wa Jimbo hilo Mchungaji David Nyambulapi .

Aliwataka  wazazi  Kuwahimiza watoto kufanya  shughuli ambazo serikali ina weza kushirikiana nao ,shughuli hizo kama vile elimu na taasisi za malezi na kuepukana na kazi zisizo kuwa na uhalali  hasa michezo hiyo ya kubashiri mitandaoni .

Pia kutumia nguvu kazi za kujiingizia kipato na kuepukana na na uvivu ,jambo ambalo litawafanya kuepukana na kufanya kazi za utapeli hasa mitandaoni ,jambo ambalo linaweza kuleta mmomonyoko wa maadili na kuzuia maendeleo ya nguvu kazi .

Hata hivyo aliwataka wataka wabunge pamoja na viongozi wa dini  kuungana pamoja Katika maswala mbali mbali ya kijamii,kiuchumi na kisiasa  katika  kudumisha amani na maendeleo ya Taifa,kwani wao wanaweza kuwa chachu kwa jamii .

Dkt.Kipangula alitoa wito kwa jamii kujikita katika  ubunifu na kujibidiisha katika kutumia fursa zilizopo katika mazingira wanayoishi mfano kutumia fursa ya kilimo kama ajira na sio adhabu .

"Hii nikutokana kwamba jamii nyingi za kitanzania zina amini kwamba kilimo ni adhabu ya walio shindwa kusoma na sio ajira jambo ambalo huleta umasikini"

Alisema ni lazima watu kutumia fursa zilizopo na pia kuacha uvivu  na lazima kutumie nguvu na tufanye kazi kwa jasho .

Kuwa kuna watu hawataki kutumia nguvu wanataka vitu rahisi sana unakuta mtu anakaa na simu yake anaingia mtandaoni anatapeli hata mamilioni kuwa huo ni  uhalifu kabisa lazima jamii ibadilike ijitumii.






Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI