Header Ads Widget

RC NJOMBE:USALAMA UTAKUWA WA KUTOSHA KWENYE VITUO VYA KUPIGIA KURA

 

Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE

Wananchi Wamehamasishwa Kujitokeza  Kwenda Kuwachagua  Viongozi wa Serikali za Mitaa Ambao Watawaongoza Kwa Kipindi cha Mika Mitano Ijayo Baada ya Serikali Kuweka Mazingira Rafiki ya Kupiga Kura Kwa Watu Wote Wenye Sifa ya Kufanya Hivyo Wakiwemo Walemavu Huku Shughuli zote za Serikali Sikisitishwa Ili Kuruhusu Wananchi Kwenda Kushiriki zoezi Hilo Muhimu.


Waziri wa Mali asili na Utalii Balozi Dokta Pindi Chana ni Miongoni Mwa Viongozi Walio Zungumza na Wananchi Mjini Njombe Katika Soko kuu ambapo Amewataka Wananchi Kwa Umoja Wao Kwa Vyama Vyote vya Siasa Kutumia Siku Hiyo Maalumu Kwenda Kupiga Kura.


Aidha Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony  Mtaka Amesema  Serikali Imechagua Siku ya Kazi Kuwa ya Mapuziko  toafauti na Hapo Awali Lengo ni  Kutoa Nafasi Kwa  Wananchi Wote pasina Kujalisha Taasisis za Kidini Ili Kushiriki Uchaguzi Huo.

Pia Mtaka amewahakikishia wananchi ulinzi wa kutosha katika vituo vyote vya kupigia kura hivyo wanapaswa kwenda kwa amani kuwachagua viongozi wanaowataka.

Baadhi ya Wananchi  Kutoka Mjini Njombe  Wamekiri Kwenda Kuwachagua Viongozi wao  Ambao Wata Waongoza Kwa  Kipindi cha Miaka Mitano Ijayo Huku Wakitoa Wito Kwa Wananchi Wengine Kuto Puuza  Jambo Hilo Kutokana na Umuhimu Wake.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI