SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge Jimbo la Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 27 Novemba, 2024 ameshiriki zoezi la kupiga kura kuwachagua Viongozi wa Serikali za Mitaa.
Dkt. Tulia amepiga kura katika kituo cha Uzunguni A (Shule ya msingi Umoja) Kata ya Sisimba Jijini Mbeya ambapo amewasihi Wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi hilo ili kupata Viongozi bora.
0 Comments