Header Ads Widget

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BIMA KUENDELEA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI


Na Matukio Daima App,Mbeya

MAMLAKA ya usimamizi wa bima  Tanzania Nyanda za juu kusini(TIRA) imesema kuwa  imejipanga kikamilifu kuendelea kutoa elimu kwa wananchi  ili kukuza soko la bima  na kudumisha ufanisi na ulinzi kwa wakata bima waliopo katika maeneo mbalimbslo hapa nchini.

Kauli hiyo imetolewa October 23,2024 na  Meneja wa Mamlaka ya usimamizi wa bima Tanzania Nyanda za juu kusini ,Neema Lutula wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya huduma za fedha kitaifa inayofanyika Jijini Mbeya katika viwanja vya Ruanda Nzovwe.

"Bima ni mkataba kati ya mkata bima na mtoa bima ili kuweza kuhakikisha athari za vihatarishi kutoka kwa mkata bima ili zisiweze kutokea ndo sababu tupo kwenye maadhimisho na tumejipanga kutoa elimu kwa umma  na kuwahasa wananchi kutembelea Banda letu kupata elimu .

Hata hivyo Meneja Lutula amesema kwamba bima hizo huwa msaada mkubwa katika kuhakikisha mkataba bima anapata kinga ya athari ya majanga mbalimbali ambayo yanaweza kumpata yeye binafsi au shughuli zake za kiuchumi .

Mmoja wa wananchi waliofika kwenye Banda la Mamlaka ya usimamizi wa bima Tanzania (TIRA)Angelina Lukosi amesema ameweza kujifunza vitu vingi baada ya kupata elimu katika banda hilo ambavyo vimemfungua na kujifunza.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI