Header Ads Widget

TANZANIA YATAJWA KUWA NA JOGRAFIA NZURI KATIKA MAWASILIANO

 




Na Pamela Mollel,Arusha 

Mkurugenzi Mkuu wa TTCL,CPA Moreni Marwa amesema Shirika hilo kupitia mkongo wa Taifa umeweza kuunganisha Tanzania na Nchi zingine  zinazoizunguka katika sekta ya mawasiliano


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha CPA Marwa anasema nchi hizo ni pamoja na  Kenya,Rwanda,Burundi,Zambia,Malawi,Uganda na Msumbiji


"Tanzania inajografia nzuri sana hivyo inatoa fursa za nchi zingine kupata mawasiliano kwa urahisi  "anasema CPA Marwa


Pia amesema shirika hilo limewezesha baadhi ya makampuni ya simu kupitia mkongo wa Taifa kutoa huduma kwa wateja wao


Aidha ameongeza kuwa mpango wa Serikali ni kuhakikisha utoaji wa huduma kidijitali ili kuongeza tija katika Taifa 


Katika kuhakikisha shirika hilo linawafikia wananchi kwa ukaribu zaidi imeanzisha huduma ya Faiba mlangoni ambayo inawapa fursa ya kupata intaneti na mawasiliano kwa wakati

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI