Header Ads Widget

MPANGO WA MINARA UCSAF KUNUFAISHA WATU MILIONI 8.5

Waziri wa habari, mawasiliano na teknolojia ya habari Nape Nnauye akiwa kwenye mnara wa airtel kijiji cha Kumbanga ambapo alizindua mawasiliano ya mnara huo uliojengwa kupitia mpango wa Mfuko wa mawasiliano kwa wote (UCSAF) katika maeneo ya vijijini yasiyo na mvuto kibiashara

Na Fadhili Abdallah, Kigoma 

Waziri wa habari, mawasiliano na teknolojia ya habari Nape Nnauye amesema kuwa wananchi milioni 8.5 watanufaika na  kuunganishwa kwenye mawasiliano ya simu za mkononi na vifaa vingine vya mawasiliano  kupitia mpango wa uwekwaji minara 758 sehemu zisizo na mvuto kibiashara kupitia Mfuko wa mawasiliano kwa wote (UCSAF)

Nape alisema hayo akianza ziara ya mikoa mitano ya  kuzindua minara ya mawasiliano ambapo alifanya kazi ya kuzindua minara miwili katika wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma ambapo alisema kuwa ujenzi wa minara


 ukaleta tija katika upatikanaji wa huduma na kuchochea maendeleo kwenye maeneo yao vijijini.

Hata hivyo Waziri huyo wa habari amewataka wazazi kuwaonya na kuwasimamia watoto wao ambao wamekuwa wakitumia vibaya uwekwaji wa minara hiyo ya mawasiliano kuzua taharuki, kuwatukana viongozi na kuharibu taswira ya nchi na viongozi.

Mtendaji Mkuu wa  mfuko wa mawasiliano kwa wote (UCSAF) Justina Mashiba (kushoto) akizungumza katika uzinduzi wa mnara wa mawasiliano katika kijiji cha Bunyambo wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma

Awali Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Justina Mashiba alisema kuwa serikali imetenga fedha kwa ajili ya uwekaji wa minara 758 maeneo ya vijijini ambayo hayana mvuto wa kibiashara kwa makampuni na kufikia Juni mwaka huu tayari minara ya mawasiliano imewashwa na inafanya kazi.

Akizungumza katika uzinduzi huo Meneja wa kanda ya Magharibi airtel, Isack Kijuu alisema kuwa uzinduzi wa mnara huo unaifanya taasisi hiyo kufikisha minara 86 ambayo imewashwa na airtel katika mpango huo chini ya UCSAF.

Waziri wa habari, mawasiliano na teknolojia ya habari akizungumza na wananchi wa kijiji cha Bunyambo  wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma wakati akizindua mnara wa mawasiliano wa kampuni ya  halotel  uliojengwa kupitia mpango wa mfuko wa mawasiliano kwa wote (UCSAF).

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI