Mbunge Kihenzile
MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kusini ambae pia ni Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile amechangia kiasi Cha Tsh milioni 5 kwa Kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ikiwa ni ahadi yake kwa sharika za Isimikinyi, Ihowanza, Maduma na Njojo.Mbunge Kihenzile ametoa mchango huo leo jumapili Julai 14, 2024 baada ya kuungana na waumini wa kanisa kwa Ibada maalumu ya kugombea Taifa na Harambee .
. Katika Kanisa KKKT Usharika wa Isimikinyi Kihenzile amekamilisha ahadi yake ya Shilingi mlioni 2 na kuongeza TSH 400,000 nyingine leo.
Fedha hizo zimewasilishwa na mwakilishi wake, Andrew Chunga Afisa Tarafa ya Malangali.
Kwa upande wa Usharika wa Ihowanza, Mh Kihenzile amechangia Tshs Milion 1.5 ikiwa ni ahadi aliyoitoa kwenye shughuli ya ununuzi Vyombo vya Muziki na fedha hizo zimewasilishwa na Diwani wa Kata hiyo Kilian Ngunguru huku katika Kanisa la KKKT Maduma, Mbunge huyo amchangia Shilingi 5







0 Comments