Header Ads Widget

WARATIBU WA MWENGE WA UHURU KAGERA WAANZA MAANDALIZI YA MAPOKEZI YA MWENGE (2024) KWA KUIKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

 .





Na Shemsa Mussa

   Kagera.

Katika hatua za kuupokea Mwenge wa Uhuru  kwa Mwaka  huu 2024  waratibu wa mbio hizo ndani ya Mkoa Kagera wameanza zoezi la ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri zote za Mkoa huo.


Akizungumza katika ukaguzi huo ulioanza kufanyika katika Wilaya ya Biharamlo,Bi Hellen Mbezi Mtaalamu na Mshauri wa Mbio za Mwenge wa Uhuru,amesema kuwa lengo la kukagua na kuitembelea miradi ni kutoa ushauri na kujua ni wapi pa kurekebisha na kutambua ubora wa utendaji kazi kwa wasimamizi wa miradi.


Amesema miradi iliyotembelewa ni miradi katika sekta  ya afya , miundombinu ya Barabara ,Maji pamoja ujenzi na ukarabati wa vyumba vya madarasa katika Wilaya hiyo ,amesema licha ya kukagua miradi pia ukaguzi huo unazingatia umbari kutoka mradi mmoja hadi mwingine.


"Hapa Kagera nipo kwa kazi nyingi  na hapa Biharamlo lazima tujikomboe ili tutoke kuwa nafasi ya mwisho na natamani Mkoa uje kuwa na nafasi ya kwanza katika kazi zote za Mwenge wa Uhuru,hivo lazima tupange ratiba nzuri na isiyochosha  na miradi iwe Bora yenye viwango,amesema Bi Hellen"


Pia Bi,Hellen amewashauri Wakurugenzi,na wasimamizi wa miradi kufanya kazi kwa kushirikiana ila Kila kilicholegwa kiweze kukamilika kwa weledi bila kuleta mkanganyiko kwa wakaguzi na jamii kwa ujumla pia amewasisitiza kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa Mwenge wa Uhuru.


"Mwenge wa Uhuru ni jambo jema na la furaha siku zote tunatakiwa hapa Kagera tuutembeze  Mwenge wa Uhuru na sio kuukimbiza,Mwenge ni furaha na faraja bwana ,na tuache visa na chuki katika kazi za Serikali na tukizembea tujue Maksi Moja ya wilaya ikidondoka basi jueni tunauangusha Mkoa mzima,ameongeza Bi,Hellen"

Mratibu Msaidizi wa Mwenge wa Uhuru Mkoa Kagera Bw Yasin Mwinory amesema Halmashauri zote za Mkoa zitatembelewa  kwa ajili ya kuona  miradi  pamoja na kutoa ushauri wa nini kifanyike  na kujipanga zaidi kwa ajili ya  Mapokeo ya Mwenge wa Uhuru.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI