Na Mwandishi wetu, Matukio Daimaapp
Wananchi wa kijiji cha Makome wafurahia kupata huduma ya maji safi mradi ambao umezinduliwa na kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Godfrey Eliakim Mnzava .
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mtwara Hamis Mashindike amesema kuwa mradi huo unaenda kuongeza kiwango cha upatikanaji wa maji katika vijiji viwili vya makome A na B.
Amesema kuwa mradi huo ulianza kujengwa Novemba 2023 na una tarajiwa kukamilika Novemba 2024 ambapo unatekelezwa chini ya usimamizi wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijjijini-RUWASA Wilaya ya Mtwara.
Amesema kuwa mradi huo unajengwa kwa thamani ya Shilingi milioni 600 fedha kutoka kutoka Wizara ya maji chini ya mpango wa lipa kwa matokeo (pforR) kwa utekelezaji wa kutumia mkandarasi m/s Kellogg constraction limited.
Mradi huo umefikia asilimia 70 na unatarajia kuhudumia wananchi wapato 1,584 kati ya hao 858 wanatoka kijiji makome na 726 wanatoka katika kijiji cha makome B ambao ulianzishwa kwa lengo la kusogeza na kuongeza kiwango cha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salam kwa wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Mtwara.
Mradi huu umehusisha ujenzi wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 50,000 kwa kila moja yenye mnara wenye mita 9 ambapo tenki moja limejengwa katika kiijiji cha makome B
Mradi huu umehusisha ujenzi wa vioski 7 vya kuchotea maji, nyumba ya muhudumu, vyumba viwili vya kuwekea mitambo ya maji ya kupeleka umeme kwenye chanzo cha maji ujenzi wa ofisi ya chombo cha watoa huduma ya maji ngazi ya jamii(CBWSO), ulazaji wa bomba za maji umbali wa km4.1.
Aidha mradi huu umezingatia sera ya maji ya kumtua mama ndoo kichwani na umezingatia umbali usiozidi mita 400 kutoka kituo kimoja cha kuchotea maji kwenda kingine.
Mradi huu utaongeza huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi kutoka asilimia 67.2 mwaka 68.2 mwaka 2023 hadi asiliam68,2 2024 mara ukapapo kamilika ambap utatua changamoto ya maji iliyokuwepo awali katika kijiji hicho.
Upatikanaji wa maji utasaidia kupungua kwa magonjwa ya mlipuko katika jamii kutoana na matumizi ya maji safi na salam hvyo kuchochea maendelea, na kutoa ajira za muda mfupi.
0 Comments