Na Mwandishi wetu, Matukio Daimaapp
Kiongozi wa Mbio Za Mwenge Kitaifa Godfrey Eliakimu Mnzava amezindua mradi wa maji manispaa ya mtwara mikindani mradi unaoenda kunufaisha wananchi 42,0000 wenye thamani ya zaidiya shilingi 588,469,723.50.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo kiongozi huyo amesema kuwa ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo baada ya kutembelea na kupitia nyaraka na matumizi ya fedha.
Amesema kuwa mradi huo umekamilika kwa asilimia 100 kwa sasa ambapo tayari wannachi wameza kunufaika na mradi huo ambao kwa muda mrefu ulikuwa unasubiriwa na wananchi.
“Serikali imeelekeza manunuzi yote ya umma yafanyike kupitia mfumo wa kidigitali wa manunuzi ya umma ambao unasimamiwa na mamlaka ya ununuzi ya umma kwa maana ya PPRA.
“Zabuni zote zinatakiwa zipitie katika mfumo wa kidigitali ambapo awali tulikuwa na TANEPS na sasa tuna NEST katika mfumo huo namna ulivyotengenezwa mzabuni anaomba zabuni moja kwa moja anaweza kuomba zabuni kidigitali ambapo utachakata na kuchukua mwenye sifa ambao unaedna kupunguza malalamiko” amesema Mnzava
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira MTUWASA Rejea Ng’ondya amesema kuwa mradi huo utanufaisha wananchi wa maeneo ya Mangamba, Mtawanya, uwanja wa ndege pamoja na Mbae ambapo zaidi ya wananchi 42,000 watanufaika.
Katika mradi huu unaosimamiwa na MTUWASA na kutekelezwa na mkandarasi Bison Engineering Company Limited ambapo ulisainiwa Septemba, 2022 na kukamilika Julai,2023 ambapo kwasa uko kwa asilimia 100 na umeshaanza kutoa huduma kwa wananchi ambapo wenye kipato cha chini wamesogezewa huduma hiyo.
“Mradi huu umeboresha na kuongeza kasi ya upatikanaji wa maji na kuboresha huduma za maji safi na salama ambapo yatapunguza changamoto mbalimbali ikiwemo magojwa ya milipuko” amesema Ng’ondya
Nae Mbunge wa Mtwara Mjini Hassan Mtenga amesema kuwa mradi huo unaenda kumaliza tatizo la maji katika maeneo hayo ambayo kwa kiasi kikubwa.
Amesema kuwa mgao huo ulikuwa ukiathiri wananchi wa mitaa hiyo ambapo kutokana na mazingira wanayoishi ilikuwa changamoto kubwa kwao.
“Ni kweli tulikuwa na changamoto na uhaba wa maji licha ya mgao hata maji hayakuwa masafi lakini sasa kukamilika kwa mradi huu tanki la lita 500,000 pamoja na mradi wa chujio tumepiga hatua kubwa na tunaendelea na uboreshaji wa mabomba ya zamani na kuleta mabomba mapya” amesema Mtenga
0 Comments