Header Ads Widget

MBUNGE (CHADEMA) AITAKA SERIKALI KUPUNGUZA MATUMIZI YASIYO YA LAZIMA.

 TAZAMA FULL VIDEO BOFYA LINK HII


NA JOSEA SINKALA.

Mbunge wa jimbo la Nkasi kaskazini (CHADEMA) Mhe. Aida Kenani, ameishauri Serikali kupunguza matumizi ya fedha kwenye miradi isiyo na ulazima au uharaka na kuelekeza fedha hizo kwenye maeneo ambayo yana hali mbaya ikiwemo ukosefu wa magari ya Jeshi la Zimamoto hapa nchini.


Hayo yamesemwa leo Alhamisi Juni 6,2024 bungeni Jijini Dodoma  na Mbunge huyo wa Nkasi Kaskazini (CHADEMA) kutoka Mkoani Rukwa wakati akichangia hoja binafsi    ya Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini (CCM) Mhe. Priscus Tarimo kuhusu halmashauri za miji na wilaya kushirikiana na jeshi la zimamoto na uokoaji katika  kutatua tatizo la upungufu wa magari ya zimamoto  pamoja na vifaa vinavyotumika  kuzima moto sanjari na uokoaji.


Mbunge Aida amesema Halmashauri zenye uwezo mkubwa kiuchumi ni vema zikashirikiana na jeshi hilo kununua vitendea kazi hususani magari ya zimamoto lakini akaiangukia Serikali kwa kuendekeza matumizi yanayozidi uwezo ikiwemo kununua magari ya kifahari ya wakuu wa Wilaya wakati maeneo mengine yakiwa na upungufu ikiwemo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.


“Jambo la kwanza ambalo naweza nikashauri kama jambo hili la kununua magari ya zima moto ni kipaumbele chetu tupunguze matumizi ambayo hayana ulazima. Mhe. Spika (Dkt. Tulia Ackson) tulipitisha hapa makadirio ya kununua ma DC zaidi ya milioni 400 , kipaumbele chetu kama  ni magari ya zimamoto kulikuwa na sababu gani yakupeleka fedha zote hizo kwenye magari ya DC", Amesema Mbunge huyo pekee wa CHADEMA kwa mujibu wa CHADEMA.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI