Mdau wa maendeleo wilaya ya Kilolo mkoa wa Iringa Aidan Mlawa ametoa msaada wa baiskeli kwa ajili ya kusaidia watu wenye Ulemavu wilaya Kilolo.
Mwenyekiti wa Chama Cha walemavu mkoa wa Iringa Shaban Shomari hivi karibuni aliwaomba wadau mbali mbali kuendelea kusaidia watu wenye Ulemavu.
Shomari alisema watu wenye Ulemavu mkoa wa Iringa wanahitaji kuungwa mkono kwa Vifaa mbali mbali kama baiskeli za kutembelea pia Vifaa vya michezo na mahitaji mengine ambayo ni muhimu kwao.






0 Comments