Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa mchungaji Peter Msigwa akiwa nje ya ukumbi wa mkutano wa Uchaguzi Chadema mkoa wa Iringa wakati Uchaguzi wa Marudio ukifanyika ukumbi wa Kartasi mjini Iringa
MSIGWA ATOA KAULI HII TAZAMA VIDEO HII
Mwenyekiti
wa Chama cha demokrasia na maendelea (CHADEMA) mkoa wa Iringa William Mungai amefanikiwa
kutetea, nafasi yake ya uenyekiti kwa kupata kura 47 huku mpinzani wake
Emmanuel Chengula akipata 34.
Uchaguzi
ulikuwa na wagombea wawili katika nafasi ya uenyekiti mkoa wa Iringa na wapiga
kura 81.
Akizungumza baada
ya uchaguzi huo, amewashuru wanachama wote waliompigia kura, huku akiwataka
wale ambao hawakumpigia kura kuunga naye kwa sasa ili kuweza kujenga chama kwa pamoja
huku akiwataka wanachama wa chama hicho kwa sasa kuvunja makundi na kuelekeza
nguvu zao katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.
“Ni
washukuru wagombea kwani ukipambana na mtu uwezo wako unaonekana, uwezo
umeonekana nusu na nyingine tuna kwenda kuonyesha uko juu kwingine” Alisema
Mungai.
Mungai pia amewapongeza
viongozi wenzake wote ambao nao wamechaguliwa katika uchaguzi wa leo, huku
akiwasisitizia uwajibikaji bora pamoja na kuwashawishi wale ambao hawajawapigia
kura kwa kushirikiana nao kwani chama hicho ni cha upendo bila uoga.
“Ni
matumaini yangu kwa hii timu ninayoiona hapa ilivyo na moyo wa ushindi tuta kwenda
kunyakuwa angalia asilimia themanini ya ushindi katika uchaguzi wa serikali za
mitaa na vijiji” Alisema Mungai.
Naye, Wakili
Msomi Emmanuel Chengula amesema anakubaliana na matokeo ya uchaguzi huo kwa
kuwa ulikuwa huru ba haki na wenye uwazi kwa wagombea wote, huku akiahidi
kuendelea kuwa mwanachama hai wa Chadema kwa kufuata sheria na taratibu za
chama hicho kwa kushirikiana na wagombea wenzake ambao wameshinda.
“Kura ambazo
nimezipata naamini ndizo nilistahili kupata, huwa tunasema safari moja inaanzisha
nyingine, kwa hiyo sehemu ambayo nimekosea naamini wakati mwingine nitakapo
gombea nitaimarika zaidi”
Wakili Chengula,
amesema ataendelea kukitumikia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kwani
bado anaimani na sera zake, na ndiyo chama pekee amewahi kujiunga hivyo kwa
sasa kazi kubwa aliyo nayo ni kuungana kwa pamoja ili kuhakikisha chama hicho
kinaenda kushika dola.
Kwa upande wake
aliyekuwa meya wa manispaa ya Iringa mjini na mwanachama wa chadema Alex Kimbe
amesema ushindi huo unaakisi matokeo ya uchaguzi wa kanda ya Nyasa ambao
unatarajiwa kufanyika mei 29 mwaka huu.
“Sisi kama
timu Mungai tunajivunia ushindi huu, na sasa kwa matokeo haya tunakwenda kushinda
uchaguzi kanda ya nyasa kwa sababu hawa walioshinda ndiyo wapiga kura katika
uchaguzi huo” alisema Kimbe.
0 Comments