Header Ads Widget

CBWSO LINDI SASA KUTUMIA MFUMO WA KIELETRONIKI KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO

 








NA HADIJA OMARY

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi.Zainab Telack amesema  kuunganisha kwa  taarifa za vyombo vya utoaji huduma ya maji ngazi ya jamii CBWSO katika ukusanyaji wa mapato kielekroniki  Utasaidia kuboresha  uendeshaji wa usimamizi wa skimu za maji vijijini kwa ufanisi mkubwa .

Telack ameyasema hayo alipokuwa anafunga kikao kazi cha kuziunganisha jumuiya hizo kwenye mfumo wa kielekroniki  wa ukusanyaji mapato yaliyofanyika huko Manispaa ya Lindi 

Amesema mfomo huo wa GePG unaojulikana kama Maji is licha ya kudhibiti upotevu wa mapato lakini pia utawasaidia watendaji wa jumuiya hizo za watumia maji kuepukana na matatizo mbalimbali ya kifedha 

"Dunia tuliyonayo sasa ni ya Sayansi na Teknolojia hivyo ili tuweze kusogea na kwenda mbali lazima tukubaliane kwamba sasa mifumo ya kielekroniki ndio ambayo itatutoa tulipo kwenda mbele zaidi"

Kwa upande wake  mratibu wa mafunzo hayo kutoka ofisi za RUWASA Makao makuu George Busunzu amesema moja ya sababu ya kuingiza jumuiya hiza katika mfumo wa kielekroniki ni changamoto za mifumo ya  ukusanyaji wa mapato 

" lakini pia tulipata hoja ya mkaguzi mkuu wa serikali ambayo tulionekana tunakusanya nje ya mfumo kwa kukusanya zaidi ya bilioni 60 katika vyombo vya watuoa huduma ngazi ya jamii"

Nae Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Lindi Mhandisi Muhibu Lubasa amesema toka wakala wa maji vijijini ulipo anzishwa mwaka 2019 hali ya upatikanaji wa maji imeongezeka kutoka asilimia 58 mwaka 2019 hadi kufikia asilimia 72 kwa mwaka 2024

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakasifu Mfumo huo utakavyokuwa na manufaa makubwa kwao

Mwisho 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI