Header Ads Widget

WAHAMIAJI HARAMU 16 MBARONI MUFINDI KWA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI

 


                       

Na Fredrick Siwale - Matukio Daika App Mufindi                                  


 WAHAMIHAJI haramu hao wamekamatwa april 06 ,2024  maeneo ya Msitu wa Luganga kata ya Sao hill  Tarafa ya Ifwagi  katika Halmashauri ya Mji Mafinga Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.   


 Kamanda wa Polisi Mkoani Iringa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACAP Allan Bukumbi  alithibitisha kuwa Wahamihaji hao haramu  walitelekezwa katika Mashamba ya mahindi baada ya kushushwa kwenye gari ambayo awali ilisomeka kwa namba STL 3999 aina ya Landcruiser  V8 yenye rangi nyeupe ambayo dereva wake aliitelekeza kwa kufunga milango na kutokomea kusiko julikana.    

                       SACAP Bukumbi alisema Wahamiaji hao ni raia kutika Nchini Ethiopia ambao bado wanashikiliwa kituoni hapo kwa uchunguzi na Upelelezi zaidi.                   


Alisema baada ya uchunguzi  wa awali ilibainika kuwa gari hiyo imesajiliwa kwa namba T.803 CVW  aina ya Landcruiser yenye namba za usajili  nambaURJ 202 - 5001217 na  injini namba IUR - FE inayomilikiwa na Said Hassan mkazi wa Tabata Dar es salaam .     

                            Katika tukio lingine SACAP Bukumbi alisema katika Oparesheni ya misako inayoendelea Polisi iliwakamata Shafii Ngailo (40)   mkazi wa Uyole Mkoani Mbeya na Neema Mwangosi (42) mkazi wa Tabata Machimbo Mkoani Dar es salaam.  

                Alisema Watuhumiwa hao walikamatwa kwa tuhuma za kusafirisha boksi 56 za Vipodozi vilivyopigwa marufuku vyenye viambata sumu vikiwa kwenye basi la kampuni ya Rungwe kutokea Mkoni Mbeya kwenda Dar es salaam.                  

  Msemaji huyo wa Polisi mkoani Iringa alisema Watuhumiwa watafikishwa Mahakanani wakati wowote Upelelezi utakapo kamilika.                         





Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI