CHAMA cha Mapinduzi (CCM )kimewaonya baadhi ya wanasiasa wanaoendesha harakati zao za kisiasa kwa kujaribu kutoa kauli za kichochezi kuacha kufanya hivyo mara moja na waendeshe siasa za ustaraabu.
Hayo yamesemwa leo Aprili 29,2024 jijini Dodoma na Katibu wa Nec Itikadi Uenezi na Mafunzo (NEC ) Amos Makalla wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema amesikitishwa na kauli zilizotolewa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lisu wakati akiwahutubia wananchi waliofika kwenye maandamano yao leo jijini Dodoma.
"Lisu ametumia maneno ya kibaguzi kwamba Rais samia ni Mzanzibar na isingekuwa Muungano hana Mamlaka ya kuhamisha watu waliopo Ngorongoro huyu ni Mzanzibar akaenda mbali zaidi akisema anayafanya haya kwasababu ni Mzanzbar"amesema Makalla
0 Comments