Header Ads Widget

WATU WAWILI WAMEFARIKI DUNIA BAADA YA KUDONDOKEWA NA LORI LA MBAO IRINGA

 

 




Watu wawili wamefariki dunia katika ajali iliyotokea eneo la Tanangozi, mkoani Iringa, baada ya kudondokewa na lori lililokuwa limebeba mbao likitokea wilayani Mufindi mkoani humo.

 

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, wamesema watu hao ambao ni mwanamke na mwanaume walikuwa wakitokea msibani eneo ambalo lipo Jirani na ajali ilipotokea, hivyo walikuwa wakisubiria usafiri pembezoni mwa barabara hiyo.

 

Jimson Sanga ni rafiki wa marehemu, Isaack Mkocha, amesema, marehemu alikuwa anatokea kwenye msiba, na wakati ajali hiyo inatokea alikuwa akisubiria usafiri wa kurudi Iringa mjini, ambapo ndipo anaishi na familia yake.

 

Katika hatua nyingine Sanga ambaye ni mkufunzi katika chuo kikuu cha Iringa, amesema licha ya kuwa marehemu ni rafiki yake pia anafanyakazi na mke wa marehemu huyo, hivyo  chuo hicho kimepata msiba.

 

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo mganga mfawidhi wa hospital ya rufaa mkoa wa Iringa, Daktari Alfred Mwakalebela, amesema march 26, 2024 majira ya saa 8 mchana walipokea miili ya watu wawili ambao ni mwanamke na mwanaume na miili yao ilikuwa na majeraha mbalimbali.

 

 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI