Home
About
Contact
Header Ads Widget
Home
News
Entertainment
Sports
Magazeti
Home
kitaifa
MADIWANI KIGOMA WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI KWA TIJA
MADIWANI KIGOMA WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI KWA TIJA
Misalaba
Friday, February 16, 2024
Madiwani wa manispaa ya Kigoma Ujiji wakiwa kwenye kikao cha kupitisha makisio ya bajeti ya mapato na matumizi ya halmashauri hiyo kwa mwaka 2024/2025
Na Fadhili Abdallah,Kigoma
Mkuu wa wilaya Kigoma Salum Kali amewataka madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma Ujiji kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa miradi katika maeneo yao ili kuwezesha miradi hiyo kuleta matokeo chanya kwa wananchi wa maeneo yao.
Kali alisema hayo katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri hiyo kilichokuwa kikipitisha makisio ya bajeti ya mapato na matumizi ya halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2024/2025.
Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa madiwani wanalo jukumu kubwa katika kusimamia ukusanyaji wa mapato ya halmashauri hasa mapato ya ndani lakini pia wanao wajibu mkubwa wa kusimamia matumizi kwenye utekelezaji wa miradi kwa wananchi.
Kwa upande wake Naibu Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji,Mgeni Kakolwa akihitimisha kikao hicho cha madiwani amewataka madiwani wa manispaa hiyo kufanya kazi kwa Pamoja wakishirikiana na wataalam ili kuwezesha halmashauri yao kupiga hatua kubwa za maendeleo.
Akisoma taarifa ya makisio ya mapato na matumizi ya halmashauri kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Mkurugenzi wa manispaa ya Kigoma Ujiji, Mwantumu Mgonja alisema kuwa halmashauri hiyo inataraia kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 37.3 ambapo makusanyo kutoka mapato ya ndani yanakisiwa kuwa shilingi bilioni 4.1 na mapato ya ruzuku kutoka serikali kuu ni shilingi 22.1 bilioni kwa ajiili ya mishahara ya watumishi.
Mgonja alisema kuwa katika makusanyo hayo wanatarajia kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni 9.9 ruzuku kutoka serikali kuu kwa ajili ya miradi ya maendeleo huku kiasi cha shilingi Bilioni moja kwa matumizi mengineyo (OC).
Mkuu wa wilaya Kigoma Salum Kali akizungumza.
Naibu Meya Manispaa ya Kigoma Ujiji Mgeni Kakolwa akifunga kikao cha baraza la madiwani la manispaa ya Kigoma Ujiji kulichopitisha rasimu ya bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka 2024/2025
Post a Comment
0 Comments
MAGAZETI
NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI
TV News
World News
UZA NUNUA NASI LEO
Subscribe Us
MATANGAZO
TIBA YA UKANDAJI WA MGONGO, KICHWA KUTOKA NEEMA BEAUTY, SPA SALOON
MAKALA NZURI ZAIDI
𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐈𝐑𝐈 𝐊𝐔𝐈𝐍𝐆𝐈𝐙𝐀 𝐌𝐈𝐅𝐔𝐆𝐎 𝐑𝐔𝐀𝐇𝐀: 𝙒𝘼𝙊𝙈𝘽𝘼 𝙆𝙐𝙍𝙀𝙅𝙀𝙎𝙃𝙀𝙒𝘼 𝙈𝙄𝙁𝙐𝙂𝙊 𝙔𝘼𝙊
Andrew Chale
Sunday, May 18, 2025
Na. Jacob Kasiri - Ruaha. Wananchi walioingiza mifugo kinyume cha sheria ndani ya Hifa…
STAY CONNECTED WITH US
Ad Space
Responsive Advertisement
Most Popular
HAYA HAPA MAJIMBO MAPYA
Monday, May 12, 2025
VIONGOZI NA WANACHAMA WA CHADEMA NJOMBE WATANGAZA KUONDOKA CHADEMA.
Saturday, May 17, 2025
RAIS SAMIA ATOA MILIONI 50 KUCHANGIA UJENZI WA KANISA KIGOMA
Monday, May 12, 2025
Contact form
0 Comments