Home
About
Contact
Header Ads Widget
Home
News
Entertainment
Sports
Magazeti
Home
kitaifa
MAGARI 13 YAKABIDHIWA SEKTA YA AFYA NJOMBE
MAGARI 13 YAKABIDHIWA SEKTA YA AFYA NJOMBE
Misalaba
Friday, February 16, 2024
Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE
Kutokana na changamoto kubwa ya uhaba wa vyombo vya usafiri katika sekta ya afya na kusababisha adha kubwa kwa wananchi pindi wanapopatwa na tatizo la dharula serikali nchini imelazimika kupeleka gari kila halmashauri ili kukabiliana na adha hiyo.
Mkoa wa Njombe umekabidhiwa magari 13 yatakayohudumu kwenye halmashauri zote sita Hospitali na Chuo cha uuguzi kibena ambapo Katibu tawala mkoa wa Njombe Judica Omary wakati wa kukabidhi magari hayo amesema yakasaidie kutatua changamoto hiyo.
Taarifa ya Mganga mkuu wa mkoa wa Njombe iliyowasilishwa na Dokta David Ntahindwa imeeleza kuwa magari hayo yatasaidia kuongeza usimamizi katika vituo vya afya na kusafirisha wagonjwa wa Dharula.
Ujumbe wa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Makete William Makufwe ni kwa madereva kuwa makini katika uendeshaji wa vyombo hivyo vya moto huku Mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Dokta Frank Mganga akikiri kuwapo kwa changamoto kubwa ya usafiri katika vituo vya kutolea huduma za afya.
Akizindua zoezi la ugawaji magari hayo Mkuu wa mkoa wa Njombe Antony Mtaka ameonya tabia za baadhi ya madereva kuyatumia magari hayo kubeba bangi,kupiga ving'ora bila sababu maalumu pamoja na ulevi utakaosababisha ajali kwenye vyombo hivyo vya moto na kwa raia.
Kwa upande wao wananchi mkoani Njombe akiwemo Francis Nindi na Christina Mzena mbali na kushukuru kwa kuletwa kwa magari hayo lakini wanaomba yawe msaada pindi wanapokumbwa na maswaibu ya kiafya huko uraiani.
Hadi sasa mkoa wa Njombe katika sekta ya afya una magari 23 yanayoendelea kusaidia wananchi katika suala la ufuatiliaji wa huduma pamoja na kusafirisha wagonjwa[Ambulance].
Post a Comment
0 Comments
MAGAZETI
NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI
TV News
World News
UZA NUNUA NASI LEO
Subscribe Us
MATANGAZO
TIBA YA UKANDAJI WA MGONGO, KICHWA KUTOKA NEEMA BEAUTY, SPA SALOON
MAKALA NZURI ZAIDI
MWENYEKITI WA CCM MBEYA MJINI ASHIRIKI HALMASHAURI KUU YA KATA YA MBARIZI ROAD AHIMIZA UWAJIBIKAJI.
Gasper
Saturday, May 17, 2025
NA MATUKIO DAIMA MEDIA Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Mjin…
STAY CONNECTED WITH US
Ad Space
Responsive Advertisement
Most Popular
HAYA HAPA MAJIMBO MAPYA
Monday, May 12, 2025
RAIS SAMIA ATOA MILIONI 50 KUCHANGIA UJENZI WA KANISA KIGOMA
Monday, May 12, 2025
VIONGOZI NA WANACHAMA WA CHADEMA NJOMBE WATANGAZA KUONDOKA CHADEMA.
Saturday, May 17, 2025
Contact form
0 Comments