Header Ads Widget

JAJI ROSE ATAKA WADAU WASHIRIKI KUBORESHA UTOWAJI WA HUDUMA ZA MAHAKAMA MTANDAO

 

Na mwandishi wetu Matukio app. Mtwara

Jaji  Mfawidhi  wa Mahakama  kuu kanda ya Mtwara Rose Ally Ebrahim amewataka  Wadau wa Mahakama kushiriki katika boreshaji mbalimbali za Mahakama ikiwemo vifaa vya TEHAMA ilikufanikisha kesi za mahakama ya mtandao.


Kauli hiyo ameitoa katika  maadhimisho ya wiki ya sheria nchini ambapo alisema kuwa maboresho hayo yataendana na UPATIKANAJI  WA haki na urekebishwaji wa Sheria  mbalimbali kupitia taasisi za Sheria na bunge. 

Amesema kuwa kutokana na maboresho yaliyofanywa wamejizatiti kupunguza mashauri na kuondoa kero ikiwemo mlundikano. 


"Ilikutatua migogoro na kuzuia mlundikano wa mashauri  katika Mahakama kwakutatua migogoro Ili kudumisha amani na utulivu na maendeleo ndani ya jamii yetu" alisema Jaji Rose

Nae Mwenyekiti wa chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) mkoa wa Mtwara  Steven Lekey alisema kuwa Ili kuwa na nidhamu Kwa mawakili hakuna budi kutungwa kwa kanuni zitakazo simamia mawakili.


 "Tandahimba Mahakama yetu tukufu  kuratibu wadau wa haki ili  nakufanyia  maboresho ya sheria na kanuni zinazosimamia nidhamu ya Mawakili ilikuwa na misingi bora zaidi ya usimamiaji wa haki za mawakili" Lekey

Kwa upande  Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba  Kanali Patrick Sawala amesema kuwa wadau wa Sheria wanapaswa kutenda haki katika majukumu yao ambapo  wananchi kuijua haki na wajibu wake wanaweza kutii sheria bila  shuruti ili amani na utulivu uendelee kuwepo nchini.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI