Header Ads Widget

HALMASHAURI WILAYA BUSOKELO YATUMIA BIL.12.5/- UTEKELEZAJI MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO

HALMASHAURI ya Wilaya ya Busokelo mkoani imepokea  kiasi cha Sh. bilioni 12,578,640,411.94 kwa ajili ya utekelezaji  miradi mbalimbali ya maendeleo na kuwezesha  wananchi  kiuchumi katika kipindi cha miaka mitatu.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo Bi.Loema Peter, alisema hayo Januari 31, 2024 wakati akiwasilisha taarifa ya manafiniko ya serikali ya awamu ya Sita kwa kipindi cha miaka mitatu katika mkutano  wa Waandishi wa Habari na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na Wakurugenzi wa Halmashauri uliyofanika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Alisema kutokana na fedha, Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo imefanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Loema alitoa mchanganuo  kuwa Katika Hosiptali ya Wilaya, halmashauri ilipokea Sh. milioni 890  kwa ajili ya ujenzi wa jengo la kuhifadhia maiti (mochari), Wodi ya Wanawake, Wodi ya Wanaume, wodi ya Watoto,jengo la upasuaj,ujenzi wa nyumba ya watumishi 3 in 1 ambapo majengo yamekamilika na yanatumika.

Aliongeza kuwa ujenzi wa Kituo cha Afya  kifunda kilichopo kata ya Lufilyo, halmashauri ilipokea  Sh. milioni 500 kwa ajili ya umaliziaji jengo la wagonjwa wa nje( OPD), Jengo la mama na mtoto, maabara, jengo la kufulia na kichomea taka. 


Mkurugenzi huyo alisema fedha hizo zilizopelekwa katika Halmashauri hiyo, oia zimetumika kujenga Zahanati mpya 9 ambazo sasa zimeongezeka kutoka zahanati 20 zilizokuwepo awali na kufikia 29.


Kuhusu viituo vya Afya alisema vilikuwa 4 kimeongezeka kimoja na kuvifanya kuwa vitano pamoja na hospitali moja ya Wilaya ambayo imeshaanza kutoa huduma kwa wananchi.


Mkurugenzi huyo alisema katika kipindi cha miaka mitatu halmashauri hiyo imetumia Sh. milioni 864.7 za mapato ya ndani kujenga zahanati katika Kijiji cha Nsoso ambayo imekamilika na inatumika, ujenzi wa Bweni la Wavulana katika Shule ya  mchepuo wa Kingereza ya  Angaza.

Alisema fedha hizo za mapato ya ndani zimetumika kuwezesha  Wananchi kiuchumi  ambapo vikundi 120 sawa na Wananchi 1,014. walinufaika.


Akizungumzia mafanikio katika sekta ya Elimu Bi. Leoma alisema kuwa katika  Idara ya Elimu Msingi zimejengwa shule mbili za msingi mpya  na kufanya ongezeko la shule kufikia 64,  Sekondari nne mpya zimejengwa na hivyo  kufanya idadi ya shule kufikia 22 kutoka 18 zilizokuwepo awali. 


Katika hatua nyingine serikali iliipatia Halmashauri ya Wilaya Busokelo Sh. 3,050,000,000 kwa ajili ya ujenzi, wa jengo la utawala ukamilishaji na kuweka  samani ambapo utekelezaji umefanyika na jengo linatumika na ununuzi wa samani upo hatua  za mwisho muda wowote zinaanza kutumika

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI