Header Ads Widget

ASILIMIA 80 YA KINA MAMA MKOA WA KASKAZINI UNGUJA NA PEMBA WANAKABIKIWA NA TATIZO LA LISHE BORA

IMEELEZWA kuwa Wastani wa asilimia 80 ya Kina mama katika Mkoa wa Kaskazini Unguja na Pemba wanakabiliwa na tatizo la Lishe linalopelekea kukithiri wa vifo na mama na Mtoto wakati wa kujifungua.


Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Kinga kutoka  Wizara ya Afya Zanzibar Dkt Salim Nassor Slim wakati akizungumza na  Waandishi wa Habari kuelekea kambi  ya matibabu itakayofanyika Mkoa wa Kaskazini  Unguja Machi 04 hadi 08 mwaka huu na kuendeshwa na Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation.

Dkt. Salim Slim amesema kuwa, Tatizo la Lishe kwa kina mama ni kubwa Visiwani Zanzibar  ambapo asilimia 80 ya Wanawake katika Mkoa ws Kaskazini Unguna na Pemba wanakabiliwa nalo huku asilimia 48 kwa Zanzibar nzima.


"Watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa na maradhi yasiyoambukizwa  kutokana na kutokuwepo kwa Lishe bora ambapo husababisha Vifo  vya kina mama na Watoto hasa wakati wa kujifungua," amesema.

"Tuendelee  kuhamasisha Lishe bora kwa Wakina mama maana madhara yake ni makubwa katika jamii na maradhi yanaongezeka na tatizo la Kuzaliwa Watoto wenye changamoto  mbalimbali linaongezeka.


Kwa upande wake  Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Maisha Bora Foundation Fatma Fumbo amesema kuwa kutokaba  na changamoto  za kinamama  Taasisi hiyo imejipanga kuonesha Kambi ya Matababu kwa siku Tano kuanzia  04 hadi 08 katika Mkoa wa Kaskazini  Unguja.


Amesema kambi  hizo zitakuwa endelevu katika Mikoa yote ya Zanzibar  na wamejipanga kuwafikia Wananchi  zaidi ya  Elfu 20.

"Sisi maisha bora Foundation  tumejikita katika mambo  Watatu, Uchumi wa Buluu, Kuimarisha Afya za kina  mama na kupambana na udhalilishaji  na Ukatili wa kijinsia na sasa tunaanza na utoaji wa Huduma  za Afya," amefafanua.


Mapema Daktari Dhamana wa Wilaya Kaskazini  A Unguja, Dk. Humid Juma Said amesema kuwa, Kambi hiyo zitahusisha Matibabu na uchunguzi  kwa maradhi mbalimbali.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS