Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa mabunge duniani IPU Dkt.Tulia Akson amewataka Wakulima nchini kuendelea kuzalisha na kupandisha thamani mazao yao kwani kufanya hivyo kutapanua soko la kimataifa na kuwa na uhakika na kilimo.
Dkt.Tulia Akson amesema hayo Mkoani Njombe katika ufunguzi wa mkutano wa 28 na maadhimisho ya miaka 30 ya Mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania MVIWATA uliokutanisha wakulima wadogo kutoka mikoa ya Tanzania na nchi mbalimbali ambapo amesema ni wakati muafaka sasa kwa wakulima kuongeza tija ya uzalishaji Ili kulisha taifa mara dufu.
Antony Mtaka ni mkuu wa mkoa wa Njombe amewataka watanzania ambao ni wakulima ,licha ya kuzalisha mazao kwa wingi wakumbuke kuwaandalia watoto wao chakula ambacho kimeongezwa virutubisho.
Mkurugenzi Mtendaji wa MVIWATA Tanzania Stephen Ruvuga akizungumza katika mkutano huo ameiomba serikali kuweka mazingira rafiki kwa wakulima wadogo ili waweze kuongeza tija katika sekta ya kilimo kwani endapo mifumo bora itawekwa itapunguza changamoto ya kupungua kwa chakula nchini.
Ruvuga pia ameomba kushughulikiwa kwa changamoto ya soko la mazao mbalimbali kwani wakati mwingine bei ya mazao imekuwa mwiba mkubwa kwa wakulima ukilinganisha na gharama ya mbolea.
Kilio cha Wakulima Mbele ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Tulia Akson Ambaye Ndiyo Mgeni wa heshima Katika Mkutano Huu ameiomba Serikali Kulichukulia Suala Hilo Kwa Uzito.
0 Comments