Header Ads Widget

WAFANYABIASHARA WAITAKA TRA KUENDELEA KUTOA ELIMU YA MASWALA YA KODI.

 


Na WILLIUM PAUL, MOSHI. 


BAADHI ya wafanyabiashara   katika  Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro,  wameitaka mamlaka  ya Mapato  Tanzania (TRA), mkoa wa Kilimanjaro  kuongeza utoaji wa elimu juu ya mlipa kodi na ufanyaji wa biashara ili kuwepo muamko wa wafanyabiashara kulipa kodi na sio kutumia vitisho kama wanavyofanya baadhi ya watumishi wao.


Akizungumza jana mara baada ya uzinduzi ya wiki ya Shukurani  kwa mlipa kodi Yashiva Shan,  alisema  asilimia 80 ya walipa kodi bado hawana utayari wa kulipa kodi na badala yake hulipa kutokana na kuogopa vitisho.


Shan alisema  wataalamu hao, wanapofika katika biashara, hawana lugha za kuelimisha na badala yake kutoa vitisho na wakati mwengine  kuwataka kulipa fidia jambo ambalo linajenga hofu.


"Leo wamesema wamefikia malengo na kuvuka,  hatuwezi kuwapa hongera kwani kwa wafanyabiashara wa mkoa wa Kilimanjaro  wangeweza kukusanya zaidi endapo wangekuwa lugha za ulimishaji,


Wakati mwingine hudai wafanyabiashara wanageuka  mimi nashauri kutokana na uhali ya utafutaji, waunde magroup  ya wafanyabiashara kutokana na biashara zao, Mfano vipodozi,  vileo   ambapo kila mara kwa kushirikiana na wataalamu  wengine wanaonyesha fursa za masoko, namna bora ya kukaribisha wateja na kisha namna ya kufunga hesabu hii ingesaidia ulipaji wa kodi kwa hiyari tofauti na ilivyo kwa sasa wanachukua wasipojua vilipotoka,"alisema Laura Mushi 


Hosiana Msuya  mfanyabiashara wa vipuli vya magari alisema licha ya wataalamu hao kutoa elimu ila  bado haikidhi hitaji la wafanyabiashara.


"Yawezekana  ikawa nje ya uwezo wao, ila ni wakati umefika serikali kutoa elimu ya mara kwa mara kwa wafanyabiasha kuhusu uzalishaji, usambazaji, uuzaji wa bidhaa ili kuleta faida itakayomuwezesha mtu kulipa kodi kwa hiyari,sio kutoa elimu ya kodi tu haimsaidii mfanyabiashara "alisema Hosiana.


Aidha  akisoma risala yake kwa mgeni rasmi Meneja wa TRA mkoa wa Kilimanjaro  James  Jilala   alisema  Mamlaka hiyo  imekusanya  zaidi ya bil.263 kwa mwaka 2022/23 ambayo ni zaidi ya asilimia 100 kutoka kwenye lengo   lilokusudiwa bil.257 kwa kipindi kilichopita.


Alisema katika mwaka wa fedha unaoendelea, tayari wamekusanya bil.71 sawa na asilimia 72 ya lengo la kukusanya bil.76 kwa kipindi cha julai hadi Oktoba 2023.


"Jitihada hizi ni ushirikiano wa pamoja kati ya watumishi pamoja na walipa kodi, ila tunakabiliwa tatizo la magendo katika maeneo mbalimbali, yakiwemo Chekereni  na Kahe hali inayopelekea upotevu wa mapato.Tunamikakati kwa kushirikiana na taasisi za kiserikali za kuhakikisha tatizo hilo linakomeshwa,"alisema Meneja.


Nae mgeni rasmi katika  wiki hiyo, mkuu wa  Wilaya ya Moshi,  Kisare Makori  alisema ajenda yankuongeza mapato ni la lazima na kuzitaka mamlaka husika kuongeza hali ya upatikanaji wa magari ya Doria ili kudhibiti  hali hiyo.


"Wafanyabiashara  tulipeni kodi hii ndio msingi wa maendeleo ya taifa letu, na ikiwa kunamatatizo katika mfuno  tuleteeni na tutayafanyia kazi kwa kuwasilisha katika ngazi husika na tatizo hilo litageuka historia," alisema Mkuu wa wilaya.

Mwisho.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI