Header Ads Widget

SERIKALI YA AWAMU YA SITA CHINI YA RAIS DKT SAMIA IMEFANYA KAZI KUBWA -JOSEPH LYATA MWENEZI CCM MKOA WA IRINGA

 


SERIKALI ya awamu ya sita chini ya Rais Dr Samia Suluhu Hassan imeendelea kuufungua mkoa wa Iringa kiuchumi zaidi kupitia Miradi mbali mbali ya kimaendeleo inayotekelezwa katika mkoa .

Akizungumza na waandishi wa Habari leo ofisini kwake katibu wa Itikadi na Uenezi na Mafunzo mkoa wa Iringa Joseph Lyata alisema ndani ya mkoa wa Iringa kuna Miradi mikubwa ya afya ,Utalii ,miundo mbinu ya barabara kiwanja Cha Ndege Iringa na Miradi mingine yenye lengo la Kukuza Uchumi wa mkoa .

Alisema mradi wa Ujenzi wa barabara ya lami Iringa- Kilolo  na Ujenzi wa barabara ya Nyololo -Kibao utakwenda kufungua Uchumi wa wananchi wa Wilaya za Mufindi na Kilolo pia mkoa kwa ujumla .

Pia alisema mradi wa Maji wa Sawala -Kibao ni mradi mkubwa wa Maji utakaomaliza kero ya Maji katika maeneo hayo .

Lyata alisema sanjari na Miradi hiyo ya Maji ipo Miradi mbali mbali ya Maji inatekelezwa kwenye maeneo mbalibali ya mkoa wa Iringa .

Kwani alisema azma ya serikali ya awamu ya sita ni kuona inamtua mama Ndoo kichwani .

Aidha Lyata alisema mradi mkubwa wa Utalii wa Regrow ni mradi utakaofungua mkoa wa Iringa kiuchumi kwa kuingiza watalii Wengi zaidi ndani ya mkoa na pindi Uwanja wa Ndege wa Iringa utakapokamilika Kasi ya Utalii Itakuwa Kubwa zaidi .

Katika hatua nyingine Lyata alionya baadhi ya wanasiasa ambao wameendelea kupita mitaani kusajili wananchi na kuwaingiza kwenye mikopo ya moto jambo ambalo chama halitawavumilia .

Alisema sensa ya watu na makazi ilikwisha fanyika na mwenye Mamlaka ya Kukusanya taarifa za Watu nchini ni Ofisi ya mtakwimu mkuu na sio chama cha Siasa .

Hivyo aliomba Vyombo Vya ulinzi na usalama mkoa wa Iringa kuwafuatilia Watu hao wanaokusanya taarifa za Watu kinyume na utaratibu wa nchi.

Alisema vikundi vya Watu hao wanaopita mitaani wanafanya kazi ya kuitukana Serikali na Rais jambo ambalo Si sawa.







Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI