Header Ads Widget

ALIYEUA WATOTO WATATU AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA NJOMBE


 Mahakama Kuu Kanda ya Iringa iliyofanya kikao chake mkoani Njombe imemuhukumu Joel Nziku kunyongwa hadi kufa, kwa kosa la kuwaua watoto watatu wa baba yake mdogo. 


Akisoma hukumu hiyo Jaji Aboubakar Mrisha amesema mshitakiwa huyo alitekeleza mauaji hayo mwezi Januari mwaka 2019 katika Kijiji cha Ikando, Kata ya Kichiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.


 Jaji Mrisha amesema mshitakiwa huyo alikwenda nyumbani kwa baba yake mdogo na kuwachukua watoto watatu ambao aliwapakia kwenye lori na baadae aliwaua kwa kuwapiga na kitu kizito na kisha kuitelekeza miili katika maeneo tofauti. 


Amesema pamoja na mshtakiwa kukana kuhusika na mauaji pamoja na kukana kutowafahamu watoto waliouawa, mahakama imesema kupitia vielelezo na mashahidi tisa walioapa na kutoa ushahidi mahakamani hapo, mahakama hiyo imemkuta mshitakiwa na hatia ya mauaji. 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI