Header Ads Widget

RTO IRINGA ATOA ELIMU KUIMARISHA USALAMA BARABARANI KWA WATOTO

 

Mosi Boniphace Ndozero; Mratibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi,
katikati aliyeshika kibao akitoa maelekezo



Na Mwandishi wetu, Iringa.


Ajali barabarani zimekithiri nchini hasa kwa Watoto wadogo wanafunzi wa shule za msingi, ili kudhibiti ajali hizo jeshi la polisi nchini kupitia kitengo cha usalama barabarani mkoa wa Iringa limekuja na mbinu mpya ambapo limeanzisha klabu za usalama barabarani shuleni.

 

Akizindua kampeni hiyo Mratibu mwandamizi wa jeshi la Polisi, Mosi Boniphace Ndozero amesema lengo ni kuwajengea uwezo wanafunzi wa shule za msingi waendelee kukua na utamaduni wa usalama barabarani, na kujua namna bora ya kutumia mfumo wa barabara kwa maana ya kuweza kuvushana watokapo nyumbani kuelekea shuleni na shuleni kuelekea nyumbani.

 

“Hii ipo makusudi kabisa ili kuwasaidia wanafunzi wasipate madhara pindi wanapotumia barabara, kwa mfano ajali ambazo zinazima ndoto zao” alisema.

 


Kampeni ya hiyo imeanzia katika shule nne ambazo ni, Tumain shule ya msingi, Ngome shule ya msingi, Maendeleo shule ya msingi pamoja na Mlangali shule ya msingi zilizopo ndani ya manispaa ya Iringa, ambapo jeshi la polisi limegawa vifaa maalumu (vinavyoitwa scholar patrol au junior patrol system) watakavyotumia wanafunzi hao wakati wa zoezi hilo la kuvushana barabara. “Kwa hiyo huu mfumo wanatumia vibao kama hivi, ambavyo tumewaelimisha kwamba wanaposimamisha magari watakuwa wanaonesha kwenye alama nyekundu watavuka na baadae watageuza upande wa kijani kuruhusu magari kuendelea na safari” amesema Ndozero.

 

Happiness Shayo; Mwalimu mkuu wa shule ya Msingu Tumain,
akiongea na waandishi wa habari

Akishukuru kwa mafunzo hayo kwa Watoto, Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Tumain, Happiness Shayo, amesema, “sisi binafsi itatusaidia kwa sababu watoto hawa ni wadogo wanahitaji kupewa uzoefu ni kwa namna gani wanaweza kuvuka barabara kwa usalama.”

 




Mwisho

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI