Header Ads Widget

BAR YA NICE BEACH RESORT, ZANZIBAR YAFUNGIWA

 


MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Ayoub Mohammed Mahmoud  ameagiza kufungiwa kwa Baa ya Nice Beach Resort  kufuatia Malalamiko yaliyotolewa na Wananchi  juu ya ukiukwaji wa Sheria na maadili.


Ayoub ametoa maagizo hayo wakati wa mkutano maalumu wa kusikiliza Kero mbalimbali kwa shehia Tatu ikiwemo Shehia ya Mangapwani, Misufini pamoja na Kidanzini katika Uwanja wa Vidimni.


Mkuu huyo wa Mkoa amesema hatua hiyo ameichukua  kufuatia kero zilizotolewa na Wananchi na kujiridhisha juu ya ukiukwaji wa Sheria, taratibu na maadili.


"Kupitia kikao hichi ndugu zangu Wananchi  nataka kuwaambia  kuwa baa imekiuka taratibu, Sheria na maadili yetu hivyo namwagiza  Kamanda  wa Polisi  wa Mkoa kuifungia baa  haraka  iwezekanavyo," Ameeleza.


Kupitia Kikao hicho  Mkuu huyo  wa Mkoa amesisitiza Wamiliki wa Baa na kumbi  za Starehe  kufuata kanuni  na Sheria  za Nchi.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI