Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE
Wakati mkoa wa Njombe ukitarajia kupokea wageni toka mikoa 31 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaotarajia kushiriki Tamasha la Utamaduni mwishoni mwa mwezi huu wa Agosti Wananchi mkoani hapa wametakiwa kutumia fursa ya tamasha hilo katika kuwaingizia kipato.
Mbele ya vyombo vya habari mkoani Njombe mkurugenzi wa Wizara ya utamaduni Sanaa na michezo Dokta Mnata Resani amesema tamasha hilo baada ya kufanyika kwa mara ya kwanza jijini Dar es salaam sasa litakwenda kufanyika mkoani humo katika viwanja vya sabasaba kuanzia agosti 25 hadi 27 mwaka huu.
Aidha Dokta Resani amesema Ujio wa wageni mbalimbali takribani 2000 toka nje ya mkoa wa Njombe uwe fursa kwa wakazi wa Njombe katika kujiingizia kipato kama wajasiriamali.
Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Njombe Kissa Kasongwa ambaye ni mwenyeji wa eneo linakofanyika Tamasha hilo amewakumbusha wananchi kuwakarimu wageni watakaofika katika shughuli hiyo.
Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa Njombe akiwemo Erick Mlelwa wamekiri kwenda kutumia fursa ya tamasha hilo katika kujiingizia kipato.
Mgeni Njoo mwenyeji apone,Kauli hii inapaswa kutafsiriwa vyema kupitia fursa ya Tamasha hilo.
0 Comments