Header Ads Widget

RPC IRINGA AWEKA WAZI WATUHUMIWA WALIOFUNGWA NA KUHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA KWA MAUAJI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa Allan Bukumbi akionesha leo kwa waandishi wa habari hawapo pichani bunduki aina Gobore iliyokamatwa katika Oparesheni iliyofanywa mkoani hapa 


JESHI la  polisi  mkoa  wa  Iringa limetaja  mafanikio  yaliyopatikana  kati ya Julai  5 hadi Julai 12 mwaka  2023  kuwa  mbali ya  kukamata  watuhumiwa  wa makosa  mbali mbali   watuhumiwa 11 waliokamatwa  na  kufikishwa  mahakamani  walikutwa na hatia akiwemo  Naftar Lyandala (40) mkazi  wa  Uhambingeto  ambaye  amehukumiwa kunyongwa  hadi  kufa kwa  kosa la mauwaji .


Akitoa taarifa  jana  kwa waandishi wa habari  kamanda  wa  polisi  wa  mkoa wa  Iringa  Allan  Bukumbi  alisema  kuwa  mbali ya  Lyandala   kuhukumiwa  kunyongwa  hadi kufa  wengine ni Francis Masoud (41) mkazi  wa  Kitasengwa , Denis  Mtega (31) mkazi wa  Ilula Mtua na Emannuel Nzogela (29) mkazi wa  Ipogolo  kwa  nyakati  tofauti  wamehukumiwa  kifungo  cha miaka 30 jela kwa makosa ya  kubaka.

 Aliwataja   watuhumiwa  wengine  kuwa ni  Godfrey Chengula (33) mkazi  wa Isakalilo  aliyehukumiwa  kifungo  cha mwaka mmoja jela kwa kosa la  kutoroka chini ya  ulinzi  , Batros  Kipako (47)  aliyehukumiwa  mwaka mmoja jela  kwa  kosa la  kupatikana na  silaha aina ya  Gobore , Musa Mtung'e (35) mkazi wa  Idodi  alihukumiwa  kifungo  cha miaka  mitano  jela kwa  kosa la  kujaribu kubaka ,Prudence Patrick (24)  mkazi  wa TRM KIhesa  alihukumiwa  kifungo  cha miaka  7 kwa  kosa la mauaji pamoja na  Desderia Mbwelwa (52) mkazi wa  Lumuli Ifunda aliyehukumiwa  kifungo  cha miaka 26 kwa  kosa la  shambulio  la aibu dhidi ya mtoto .

Kamanda  Bukumbi  alisema Emmanuel  Mahundi (31) mkazi  wa  kijiji cha Ibumu wilaya ya  Kilolo  alihukumiwa  kifungo  cha  maisha  jela kwa  kosa la kubaka pamoja na fidia ya shilingi  500,000 huku Godi  Kasungula (41) mkazi  wa Ipilimo  wilaya ya  Mufindi  akihukumiwa  miaka  30  jela kwa  kosa la unyang'anyi  wa  kutumia  silaha .


Pia  alisema  katika  oparesheni  ya  kuthibiti  magari yanayotembea  usiku  kwa  kutozingatia  sheria  jeshi la  polisi  lilifanikiwa  kukamata  magari  12  kwenye oparesheni  hiyo   iliyofanyika mkoani hapa  kati ya Julai 5 hadi Julai 12 mwaka huu  na  kuwachukulia hatua  za kisheria  madereva  kwa  kushindwa kuzingatia  sheria  za usalama  barabarani  ikiwa ni pamoja na  kuendesha  magari ya  abiria  bila  leseni ya  usafirishaji  kukosa  ratiba za  safari  na makosa  mengeni ya  kiusalama  barabarani .

Aidha   jeshi  la  polisi Agost 8 mwaka  huu lilimkamata  Jacob Mhanga (54) mkazi  wa  Kijiji  cha Utiga mkoa  wa Njombe akiwa na vipande saba  vya meno ya Tembo  katika  nyumba ya kulala  wageni  iliyopo  kijiji  cha  MBalamaziwa  kata ya Kasanga wilaya ya  Mufindi  kuwa mtuhumiwa  huyo  atafikishwa mahakamani  pindi  upelelezi  utakapokamilika.


Bukumbi   alisema katika  misako  mbali mbali inayoendelea jeshi la  polisi  kwa  kushirikiana na askari  wa  Uhifadhi kwa  kupokea  taarifa  fiche   kupitia  Raia  wema   Agost  6  mwaka  huu majira ya  saa moja  usiku  walifanikiwa  kumkamata Mathias Malenga (37) mkazi  wa  kijiji cha Image   Tarafa ya  Mazombe wilaya ya  Kilolo  akiwa na silaha  mbili ndani ya nyumba yake moja  ikiwa ni  Shortgun   isiyo na namba  ikiwa na risasi  mbili na maganda matatu  na nyingine  ni  Gobore  moja na Goroli  sita  pamoja na  mtego  wa  kuwindia wanyama kuwa mtuhumiwa  huyo  atafikishwa mahakamani .


Kati  hatua  nyingine kamanda  Bukumbi  alisema  kupitia   oparesheni  iliyofanyika  Juni 7 hadi Julai 10 mwaka  huu jeshi la  polisi  mkoa  wa  Iringa  lilifanikiwa  kuwakamata watuhumiwa  tisa  wa makosa mbali mbali  ya  kuvunja na kuiba ambao ni  Samweli Malila mkazi wa  Kinyanambo  C Mafinga  wilaya ya  Mufindi , Fahamu  Msisi (40) mkazi wa Mji Mwema  Mafinga ,Satoki  Sanga (50) mkulima wa Luganga ,Steven  Peter (43) mkazi wa Mafinga , SAid Degele(24) mkazi wa Mwangata ,Joshua Elihuruma (42) mkazi  wa Kitanzini na Goodluck Mpangile (25).

Alisema  watuhumiwa  hao  walikamatwa wakiwa na mali mbali mbali zi;nazodhaniwa  kuwa  za  wizi  ambazo ni  pikipiki nne zenye  namba za usajili  MC 473 AAP na MC 294 DPG zote aina ya  Haojue pia  pikipiki aina ya SUNLG yenye  namba  Chasis LBRSPKB5509004894 na PIkipiki matairi matatu MC 724 DHJ.

Vitu  vimngine  walivyokamatwa navyo  ni pamoja na  TV moja  aina  ya  EVVOL yenye S/N 0C15 na  NM 1DK140985-00838,MN 32EV100,Laptop mmoja  aina ya SnSV yenye   S/N  0C15 na  M/N 9461D2W  jeki  moja  ya gari  na  spana  mbali  mbali pamoja  na Extension Cable  mbili ,Blankent moja  ,magodoro  mawili  na  vitu mbali mbali  vya  dukani  kama  Cherehani na  vingine  vingi .

Hata  hivyo  kamanda  Bukumbi  mbali ya  kuwashukuru  wananchi  wanaoendelea  kuchukizwa na  watu  wanaojikhusisha na uhalifu na   matukio ya  uhalifu  bado  aliomba  raia  kuendelea   kutoa  ushirikiano  zaidi kwa  jeshi la  polisi  kwa  kuwafichua   wahalifu na uhalifu .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI