
Meneja wa CPB kanda ya nyanda za juu kusini Dkt Jaspa Samweli alimweleza mwandishi wa matukio Daima Media leo kuwa ongezeko la wakulima wakubwa na wadogo kuuza mazao kwa sasa ni kubwa zaidi kwani imepelekea zoezi la ununuzi wa mahindi kuongezwa kasi zaidi ikiwa ni pamoja na kuongeza vituo vya ununuzi wa mahindi hayo katika mikoa ya Singea mkoa wa Ruvuma , Mlowo na Tunduma mkoa wa Songwe Songwe pamoja na Iringa .
Alisema kuwa CPB imeanza kununua mahindi mwezi mmoja uliopita kwenye kituo cha Iringa kwa Julai 24 bei ya mahindi kwa kilo moja ni kiasi cha shilingi 950 wakati kituo cha Songea kwa kilo ni shilingi 850 kwa kilo kituo cha Mlowo na Tunduma mkoani Songwe kilo moja ni shilingi 850 .
Alisema kuwa hadi sasa zaidi ya tani za mahindi ya wakulima 13,500 zimekwisha nunuliwa kati ya tani 80,000 zinazotarajiwa kununuliwa kutoka kwa wakulima ndani ya mikoa ya nyanda za juu kusini .
Hata hivyo alisema kutokana na ongezeko kubwa la wakulima kukimbilia kuuza mahindi yao katika ofisi za CPB Iringa wamelazimika kuweka utaratibu wa kununua mahindi hayo kutoka kwa wakulima wa gunia mpoja hadi tani mbili na wale wakulima wakubwa wa tani saba na kuendelea ambao wanafika kuuza mahindi yao .
Alisema kwa wote wanaofika kuuza mahindi yao kuwa viwango vya ubora wa mahindi yanayotakiwa kununuliwa hivyo kabla ya ununuzi mahindi yanapimwa maabara na yale yaliyokidhi viwango yananunuliwa kwa mkulima kuingiziwa pesa yake katika akaunti ya benki zoezi ambalo linachukua muda mfupi zaidi toka ununuzi
Dkt Samweli alisema kuwa eneo la ununuzi wa mazao linauwezo wa kupokea magari 50 kwa wakati mmoja japo kwa sasa magari yanayoingia kwa wakati mmoja ni kati ya 100 na zaidi hivyo wameweka utataribu mzuri wa kuona kila mkulima anauza mahindi yake CPB kwa wakati zaidi .
Alisema wakulima wanaofika kuuza mahindi baada ya kufika mahindi yanachukuliwa sambo pamoja na namba ya gari jina la dereva na namba yake ya simu kisha dereva anaruhusiwa kwenda kuegesha gari lake sehemu yoyote ndani ya mji wa Iringa na pale majibu ya vipimo vya maabara yatakapotoka dereva anapigiwa simu ili kuingiza gari kwa ajili ya upakuaji wa mzigo na wale ambao watakuwa hawajakidhi vigezo kwa mahindi yao kukosa ubora wamekuwa wakijulishwa ili kwenda kutafuta soko sehemu nyingine .
Dkt Samweli alisema kuwa mwitikio mkubwa wa wakulima kufika kjuuaza mazao yao kwao ni kutokana na bei nzuri ya ununuzi wa mahindi kwa kilo kwani mtaani wafanyabiashara wananunua mahindi kwa kilo kwa kiasi cha shilingi 650 kwa kilo hivyo alisema bado anatoa rai kwa wakulima na wafanyabiashara kuendelea kutumia fursa ya kuuza mahindi CPB bora mahindi yawe na ubora .
Alisema CPB ina jumla ya vipimo 12 vya kupima ubora wa mahindi yanayonunuliwa ili kuendena na soko la mahindi la Afrika Mashariki ili kuepuka kulichafua Taifa kwa kupeleka mahindi ama unga usio na ubora katika soko la Afrika Mashariki .
" Uandaaji wetu wa mahindi toka kwenye ununuzi hadi usagaji ni uandaaji wenye viwango vya soko la Afrika mashariki ambao unatumiwa na nchi zote za Afrika mashariki pia alisema mfano unga unaotoka CPB ni unga wenye virutubisho vyote na unga usio na madhara ya Sumu kuvu "
Alisema kama mahindi ama unga ama maharage na mazao mengine yanayotoka Tanzania yakipelekwa nje ya nchi na kubainika kuwa na tatizo aibu hiyo si ya wakulima ama CPB pekee yao bali ni aibu kwa Taifa zima na atakayeangaliwa na Rais wa nchini ya Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan na sio mkulima ama CPB hivyo ni jukumu lao kuendelea kulinda taswira ya nchi kwa kuzingatia ubora wa mazao yanayonunuliwa na kuuzwa nje ya nchi.
0 Comments