Header Ads Widget

AJALI YA BASI LA KAMPUNI YA NEW FORCE KITONGA

 





ABIRIA 57 waliokuwa wakisafiri na basi la kampuni ya New Force kutoka Mbeya Kupeleka Dar es salaam wamenusurika kifo baada ya basi Hilo kupinduka Katika Mlima Kitonga mkoani Iringa .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, ACP Allan Bukumbi amethibitisha kutokea Kwa ajali hiyo na kuwa basi hilo lenye usajili namba 

T448DDT Zong Tong  Mali ya Kampuni ya  NewForce Enterprises Ltd  kuwa 

 abiria wake wote 57  wako salama na hakuna majeruhi yeyote katika ajali iliyotokea eneo la Mlima Kitonga wilaya ya Kilolo barabara kuu ya Iringa Morogoro baada ya basi la Kampuni ya New Force kupinduka na kulalia upande mmoja Kando ya barabara.


Ajali hiyo ilitokea  saa 3:30 asubuhi leo Julai 2, 2023 ambapo basi hilo aina ya Yutong lilikuwa limebeba abiria 57  likitokea mkoani Iringa kuelekea jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Matukio Daima Media Kwa Njia ya simu  Kamanda Bukumbi amesema basi hilo lilipinduka na kuegama pembezoni mwa barabara wakati dereva akiyapita mabasi mengine yaliyokuwa yanateremka katika mlima huo yakiwa kwenye foleni.



"Ajali imetokea asubuhi ya Leo eneo la Kitonga wakati dereva wa basi Hilo akitaka kulipita gari jingine hakuna madhara makubwa Kwa abiria"

Alimtaja dereva Wahid  Juma Athuman , (46)mkazi wa Mbezi Jijini Dar es Salaam kuwa ndie alikuwa akiendesha basi Hilo na kulazimisha kuyapita Magari Mengine yaliyokuwa Katika Foleni kwenye mteremko wa Mlima wa Kitonga .
 
Alisema kuwa chanzo Cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva na kuwa atafikishwa mahakamani Kwa Kosa la uzembe 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI