Header Ads Widget

TULIA MARATHON YACHOCHEA FURSA ZAKIUCHUMI

 





Na  Matukio Daima Media,Mbeya


UWEPO  wa mbio za Tulia Marathon  mkoani Mbeya zimeelezwa kuchochea fursa za kiuchumi  kwa wafanyabishara kutokana na   mwingiliano mkubwa wa watu kutoka mikoa mbalimbali  na raia kutoka  nchi jirani ya Kenya.



Diwani wa Kata ya Majengo na Mwenyekiti wa Chama cha  riadha Mkoa wa Mbeya ,Maulid Jemedali wakati akizungumza na Matukio daima amesema hayo leobkatika viwanja vya kumbukumbu ya Sokoine Jijini Mbeya ikiwa ni siku ya kwanza ya mashindano hayo.


Jemedali amesema kuwa uwepo wa mbio hizo umekuwa chachu ya kuchangia shughuli miradi ya Maendeleo ya Serikali ikiwepo sekta ya elimu na afya jambo ambalo inaongeza tija katika utoaji huduma bora kwa jamii.



"Kwa Jiji la Mbeya tunaona mambo mengi ya utekelezaji wa miradi ya Maendeleo katika Sekta ya elimu na afya yanafanywa kupitia fedha zinazopatikana kupitia mashinsano ya mbio za Tulia Marathoni "amesema.



Joshua Mwakanolo ni Ofisa habari na mawasiliano wa  Taasisi ya Tulia Trust amesema kuwa Mbeya Tulia marathon lengo lake kubwa ni kuboresha miundombinu  ya elimu na afya na kwamba huo ni msimu wa saba toka kuanzishwa kwa Mbeya  Tulia Marathon.



‘’Kwa kumbukumbu  kwa mwaka 2022 Mbeya Tulia Marathon fedha iliyopatikana ilipelekwa kwa ajili ya  ujenzi wa mabweni  ya  shule ya Sekondari ipinda wilayani Kyela  baada ya hapo yalijengwa madarasa mawili shule ya sekondari Lyoto  pamoja na ofisi  ‘’amesema.



Ameongeza kuwa ‘’Hata mwaka huu tunategemea kwamba fedha itakayopatikana tutaangalia jinsi  gani tunaweza kujigawa  ili kuweza kuboresha miundo mbinu ya afya na elimu sababu tunaona kuna mwitikio mkubwa  hata uandikishaji kwani kati ya watu 4,000 waliojitokeza 14,kutoka nchi jirani ya Kenya’’ amesema.



Amesema kuwa mashindano hayo yamekuwa na mchango mkubwa sana kwa jamii hususan kuchangia ukuaji wa kipao cha mtu mmoja mmoja na vikundi wakiwepo wafanyabishara wa viatu,nduo,mama lishe na wauzaji wai vileo’’amesema 



Tulia marathon imekuwa msaada mkubwa kwa wajasiliamali  wa  mkoa wa Mbeyakwani itaweza kukuza uchumi.


Sophia Mwanautwa ni Diwani wa  vitimaalum Kata ya Makongolosi amesemakuwa lengo kuu la tulia marathon ni kuboresha elimu na afya hivyo  spika wa Bunge amekuwa akipenda maendeleo  na akizungumzia elimu na anafanya kwa vitendo.


Mh. Mwanauta amesema kubwa wana Mbeya wanapoona Mh. Spika anafanya jambo wamuunge mkono na kumpa sapoti  ili aweze kufanya vitu vya maendeleo.


‘’Kwasababu kujiandikisha sio lazima ukimbie mbio mimi hapa nimejiandikisha nakimbia kilometa tano(5)  na namba yangu ni 0368 sio kwamba kesho nitakimbia ila nimechangia kumsapoti Mh. Spika na mbunge wa jimbo la Mbeya , nawaomba wana chunya mwakani wajitokeze kwa wingi ili kumuunga mkono mwana mama huyu katika juhudi zake za kuboresha elimu kwa mkoa wa Mbeya’’amesema Mh. Diwani huyo.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI